Mbowe ahukumiwa mwaka mmoja

MAHAKAMA 
ya wilayani Hai mkoani Kilimanjaro, imemtia hatiani na kumhukumu 
Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe kwenda jela mwaka mmoja au
 kulipa faini ya Sh milioni moja, kutokana na kesi iliyokuwa ikimkabili 
ya kumshambulia mwangalizi wa ndani wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.
Akisoma 
hukumu hiyo iliyohudhuriwa na wabunge wengi wa Chadema, Hakimu Mkazi 
Mfawidhi, Denis Mpelembwa, alisema mahakama imemkuta Mbowe na hatia, 
hivyo kutakiwa kutumikia kifungo cha mwaka mmoja jela au kulipa faini 
kiasi cha Sh milioni moja.
Mbowe 
ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Hai, katika kesi hiyo ya jinai namba 73
 ya mwaka 2011, alidaiwa kumshambulia Nassir Yamin, katika Kijiji cha 
Nshara, kata ya Machame Kaskazini, Wilaya ya Hai, katika uchaguzi mkuu 
wa mwaka 2010. Mpelembwa alisema mahakamani hapo kuwa hukumu iliyotolewa
 mahakamani hapo imezingatia ushahidi uliotolewa kwa upande wa 
mlalamikaji Nassir Yamini. (DK)
        
Kwa 
upande wake, Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe akizungumza mahakamani hapo, 
alisema hukumu iliyosomwa mahakamani hapo haijamtendea haki.
Alisema 
kesi yake hiyo haikustahili kuchukua muda mrefu kama mahakama 
ilivyofanya kwa kuchukua zaidi ya miaka mitano bila kusomewa hukumu.
Hata 
hivyo, Mbowe amelipa kiasi cha fedha Sh milioni moja alichotakiwa kulipa
 kama hukumu ilivyoeleza, kwa kumtaka kulipa kiasi hicho cha fedha au 
kwenda jela mwaka mmoja.
Lema na Polisi
Wakati 
Mbowe akihukumiwa, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema jana alishindwa
 kuzuia hasira zake na kutaka kupigana na mmoja wa askari polisi katika 
kituo cha kuandikisha wapigakura cha Mkombozi kata ya Sokoni One, Jimbo 
la Arusha.
Tafrani 
hii ilitokea baada ya kukuta polisi huyo akiandikisha wananchi 
wanaohitaji vitambulisho, kabla ya kuingia ndani ya chumba cha 
waandikishaji.
Vurugu 
hizo zilitokea saa 5:30 asubuhi, mara baada ya Lema kuingia eneo hilo 
akitembelea vituo vya kuandikisha wapiga kura kuangalia hali halisi.
Alipofika
 kwenye kituo hicho alikuta mmoja wa Polisi akiwa amevaa kiraia (Jina 
halikupatikana mara moja), akiwa na daftari dogo akiorodhesha majina ya 
wapiga kura kwa lengo la kupunguza foleni.
Akizungumza
 na wananchi huku Lema akiwa amezungukwa na askari polisi, alisema huo 
sio utaratibu wa kufanywa na polisi na hata Tume hairuhusu Polisi 
kufanya kazi hiyo bali kulinda amani tu.
Hata 
hivyo, Mkuu wa Kituo Kikuu cha Polisi cha Arusha, Thomas Maleko, 
akimtuliza hasira Lema akisema wao wanafanya kazi hiyo, ili kuwapunguzia
 adha wananchi ambao wanafika kituoni saa 9:00 usiku, hadi siku ya pili 
wanakaa kutwa nzima bila kupata fursa ya kuingia chumba cha 
kujiandikisha.
Alisema 
kutokana na hali hiyo, ndipo Polisi walipoamua kuandikisha watu kwa 
makubaliano na waandikishwaji wenyewe, ili waondoke nyumbani wakafanye 
kazi zingine na kesho yake wakirejea wanapata fursa hiyo.
“Hawa 
watu hata wakikaa hapa hawawezi kuingia ndani ya chumba husika, maana 
kuna kompyuta moja tu, hivyo wanapigwa na jua, hivyo utaratibu huu sisi 
tumeona ni mzuri, tunaandika jina la mtu kisha tunamruhusu aende 
nyumbani hadi kesho aje anaingia ili kupata kitambulisho,” alisema.
Hata 
hivyo, licha ya maelezo ya polisi, Lema hakukubaliana nayo na 
kuwasiliana na Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Juma Idd ambaye alimtuma 
Mjumbe wa Tume ya Uchaguzi, ambaye naye hakutaka kuzungumza chochote na 
waandishi wa habari na pia hakutaka kutaja jina lake. (HABARI LEO)
No comments:
Post a Comment