TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, June 11, 2015

Newcastle imempa ulaji kocha wa zamani wa Uingereza

2983C15200000578-3118358-Steve_McClaren
Newcastle United imemtangaza Steven McClaren kuwa kocha mpya wa klabu hiyo baada ya kumtimua kocha wake John Carver aliyenusurika kukishusha daraja kikosi hicho cha St James Park.
McClaren mwenye umri wa miaka 54 anachukua nafasi ya John Carver ambaye alifukuzwa siku ya Jumapili iliyopita, kocha huyo wa zamani wa Uingereza pia amewekwa katika bodi ya timu hiyo.
McClaren amepewa kandarasi ya miaka mitatu ambayo huenda ikaongezwa na kufikia miaka nane endapo ataisaidia klabu hiyo kutwaa taji lolote kwenye muda huo wa miaka mitatu aliyopewa kwa sasa.
Kocha huyo amesema; “nimeheshimiwa kuteuliwa kuwa kocha mkuu wa Newcastle United FC. Hii ni klabu kubwa yenye urithi wa kipekee”.(P.T)
“Mashabiki wake ni watulivu na wana moyo na timu yao, mbali na yote bado wamekuwa ni waaminifu. Tutafanya kadri tuwezavyo tuwazawadie mafanikio”, amesema.
“Kuna kazi kubwa ya kufanya, lakini klabu imeweka bayana kwamba inahitaji mafanikio, na nisingekuja hapa kama ningekuwa siamini kama wapo makini. Timu hii imekaa kwa muda mrefu bila kushinda taji lolote, na kushinda taji ndio lengo langu la kwanza kabisa hapa”, ameongeza.
“Nimeshashinda mataji nikiwa kama kocha, timu kama Newcastle United inatakiwa kushinda vikombe na kumaliza msimu wa ligi kuu ikiwa kwenye nafasi nane za juu. Nitawapa mashabiki wa Newcastle kitu ambacho watakuwa wakijivunia, na kazi hiyo inaanza sasa”, alimaliza.
Kocha huyo wa zamani wa Uingereza ambaye alipigwa kalamu na klabu ya Derby County mwezi Mei, aliikataa kazi hiyo mara mbili baada ya Alan Perdew kuondoka na kabla ya kukamilika kwa mechi tatu za mwisho za msimu huu.

No comments:

Post a Comment