Newcastle imempa ulaji kocha wa zamani wa Uingereza

Newcastle
 United imemtangaza Steven McClaren kuwa kocha mpya wa klabu hiyo baada 
ya kumtimua kocha wake John Carver aliyenusurika kukishusha daraja 
kikosi hicho cha St James Park.
McClaren 
mwenye umri wa miaka 54 anachukua nafasi ya John Carver ambaye 
alifukuzwa siku ya Jumapili iliyopita, kocha huyo wa zamani wa Uingereza
 pia amewekwa katika bodi ya timu hiyo.
McClaren 
amepewa kandarasi ya miaka mitatu ambayo huenda ikaongezwa na kufikia 
miaka nane endapo ataisaidia klabu hiyo kutwaa taji lolote kwenye muda 
huo wa miaka mitatu aliyopewa kwa sasa.
Kocha 
huyo amesema; “nimeheshimiwa kuteuliwa kuwa kocha mkuu wa Newcastle 
United FC. Hii ni klabu kubwa yenye urithi wa kipekee”.(P.T)
        
“Mashabiki
 wake ni watulivu na wana moyo na timu yao, mbali na yote bado wamekuwa 
ni waaminifu. Tutafanya kadri tuwezavyo tuwazawadie mafanikio”, amesema.
“Kuna 
kazi kubwa ya kufanya, lakini klabu imeweka bayana kwamba inahitaji 
mafanikio, na nisingekuja hapa kama ningekuwa siamini kama wapo makini. 
Timu hii imekaa kwa muda mrefu bila kushinda taji lolote, na kushinda 
taji ndio lengo langu la kwanza kabisa hapa”, ameongeza.
“Nimeshashinda
 mataji nikiwa kama kocha, timu kama Newcastle United inatakiwa kushinda
 vikombe na kumaliza msimu wa ligi kuu ikiwa kwenye nafasi nane za juu. 
Nitawapa mashabiki wa Newcastle kitu ambacho watakuwa wakijivunia, na 
kazi hiyo inaanza sasa”, alimaliza.
Kocha 
huyo wa zamani wa Uingereza ambaye alipigwa kalamu na klabu ya Derby 
County mwezi Mei, aliikataa kazi hiyo mara mbili baada ya Alan Perdew 
kuondoka na kabla ya kukamilika kwa mechi tatu za mwisho za msimu huu.
No comments:
Post a Comment