Mikoa ya Shinyanga na Mwanza yaendelea na ubabe mbio za baiskeli

Mshindi
 wa mbio za Acacia Tufanikiwe Pamoja Lake Zone Cycle Challenge, Masunga 
Duba aliyeinua mikono akishangilia mara baada ya kumaliza mbio hizo 
akiwa mbele ya wenzake. Mshindi huyo anatoka mkoa wa Shinyanga.

Mmoja wa washiriki wa mbio hizo akinywa maji wakati wa mashindano hayo.

Washiriki wa mbio za Acacia tufanikiwe pamoja lake zone cycle challenge wakimenyana vikali wakati wa mashindano hayo. (DK)

Makamu
 wa rais wa Kampuni ya Uchimbaji wa dhahabu ya Acacia, Deo Mwanyika (wa 
kwanza kushoto) akifurahia jambo na Afisa Mkuu wa Uendeshaji wa kampuni 
ya Acacia, Mishel Ash, (wa pili kutoka kushoto) ambaye pia ni kaimu 
Meneja Mkuu wa Mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu.

Washindi
 wa mbio za wanawake (kilometa 80). Aliyesimama katikati ni Martha 
antony ambaye ndio aliibuka mshindi wa kwanza, akifuatiwa na Laulensia 
Luzuba, (mwenye mtoto) aliyekuwa mshindi wa pili na Veronica Saimon (wa 
kwanza kushoto) aliyejinyakulia nafasi ya Tatu.

Afisa
 mkuu wa uendeshaji wa kampuni ya Acacia Mishel Ash akimvisha medali 
mshindi wa mbio hizo Martha Antony wakati wa Hafla ya Kutoa zawadi kwa 
washindi.
Washiriki
 wa mbio za baiskeli zijulikanazo kama “Acacia Tufanikiwe Pamoja Lake 
Zone Cycle Challenge” kutoka mikoa ya Shinyanga na Mwanza wameendelea 
kuudhihirisha umma wa wakazi wa kanda ya ziwa na watanzania kwa ujumla 
kuwa mpaka sasa hawana mpinzani baada ya washiriki wa mbio hizo kuibuka 
kidedea katika fainali za kumtafuta mshindi wa kanda hiyo.
Washiriki
 wa mikoa hii miwili wamejinyakulia nafasi zote za juu na hivyo 
kuwashinda wenzao wa mikoa mingine ya Kanda ya ziwa ikiwemo Kagera, 
Mara, Geita na Simiyu.
Katika 
mbio za wanaume za umbali wa kilometa 156.6 kutoka Kahama mpaka Tinde na
 kisha Kurejea Kahama, mshindi wa mwaka jana Masunga Duba (Mwanza) 
aliibuka tena kidedea huku nafasi ya pili ikichukuliwa na Lupilya 
Hamis(Shinyanga) na nafasi ya tatu ikimuendea Kulwa Tuki(Shinyanga), 
washindi hawa wamejinyakulia kitita cha pesa taslimu Sh1,500.000/- kwa 
mshindi wa kwanza, Sh1,200.000/= mshindi wa pili na Sh800,000/= kwa 
mshindi wa tatu.
Kwa 
upande wa mbio za wanawake za umbali wa kilometa 80, kutoka Kahama mpaka
 Mwakata Kisha kurejea Kahama, timu ya mkoa wa Mwanza imedhihirisha kuwa
 wao bado ni mabingwa kwa kuibuka tena washindi wa mbio hizo, huku 
mshindi wa mbio za Mwaka jana Martha Antony, akiibuka mshindi wa kwanza 
akifuatiwa na Laulensia Luziba na nafasi ya tatu ikienda kwa Veronica 
Simon. Washindi hao wamepata zawadi ya pesa taslimu Sh1,200.000/= kwa 
mshindi wa kwanza, Sh800,000/= mshindi wa pili na Sh600,000/= mshindi wa
 tatu.
Mbio hizo
 ambazo zimeandaliwa na Chama cha Baiskeli Tanzania (CHABATA) kwa 
udhamini wa kampuni ya uchimbaji wa Madini ya Acacia, inayomiliki migodi
 ya North Mara, Bulyanhulu na Buzwagi, yote ikiwa mikoa ya kanda ya 
ziwa, kupitia mpango wake wa Tufanikiwe Pamoja ikiwa ni mara ya pili 
sasa ambapo mashindano ya mwaka huu yameonyesha mafanikio makubwa 
kutokana na maandalizi mazuri yaliyofanyika.
Akizungumza
 na washiriki wa mashindano hayo Mkuu wa wilaya ya Kahama Benson Mpyesa,
 ambaye alikua mgeni rasmi wa fainali hizi, amesema ana imani  kuwa 
mashindano hayo yatasaidia kuibua vipaji ambavyo vitauletea sifa mkoa wa
 Shinyanga, Kanda ya ziwa na hata taifa kwa ujumla kwani baiskeli kwa 
maeneo hayo ndiyo jadi yao.
Awali 
akimkaribisha Mkuu wa wilaya kuzungumza na washiriki hao, Makamu wa Rais
 wa Acacia Deo Mwanyika amesema kampuni ya Acacia imekuwa ikifanya 
shughuli za uchimbaji unaojali na ndio maana iliona vyema kuweka 
udhamini wake pia katika mchezo wa baiskeli, “toka tuanze huu sasa ni 
mwaka wa pili na tunayaona mafanikio makubwa kwani hata maeneo ambapo 
mchezo huu ulikuwa hauchezwi sasa unachezwa, hali ambayo imeongeza 
hamasa na idadi ya washiriki.”
Aidha
 Makamu wa Rais huyo wa Acacia amesema mipango ya kampuni kwa sasa ni 
kuona pia inashiriki katika kuendeleza michezo mingine ikiwemo na soka
No comments:
Post a Comment