TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, May 20, 2015

Wahamiaji kujadiliwa,Malaysia 

Wahamiaji huko Indonesia
Mawaziri wa mambo ya nje wa Thailand,Malaysia na Indonesia wanafanya mkutano wa dharula mjini Kuala Lumpur kujadili tatizo la wahamiaji haramu katika ukanda wao.
Nchi hizo tatu zinakabiliwa na shinikizo la kimataifa kuwasaidia maelfu ya wahamiaji waliokwama Baharini ambao wanahitaji chakula na maji.
Wahamiaji wengi ni waislamu wa jamii ya Rohingya waliokimbia Myanmar, lakini Serikali ya nchi hiyo imekataa kuhudhuria mkutano huo.
Wavuvi nchini Indonesia wamewaokoa zaidi ya wahamiaji 100 siku ya jumatano
Bado kuna hofu kuhusu usalama wa waliokwama baharini.Maelfu ya Raia kutoka Bangladesh na Waislamu jamii ya Rohingya wamekuwa katika bahari ya Andaman kwa majuma kadhaa sasa.
Thailand,Malaysia na Indonesia zimekataa kuwaruhusu kuingia katika pwani za nchi zao.CHANZO:BBC (Muro)

No comments:

Post a Comment