TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, May 13, 2015

Lissu achafua hewa bungeni 

Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu akizungumza bungeni wakati wa kupitisha Muswada wa Sheria ya Miamala ya Kielektroniki wa Mwaka 2014 na Sheria wa Makosa ya Mtandao wa Mwaka 2015 mjini Dodoma, juzi usiku. Picha na Anthony Siame.
Dodoma. Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu jana alichafua hali ya hewa bungeni baada ya kudai kuwa Serikali ya Awamu ya Nne ni ya kichovu, kauli ambayo ilizua mabishano makali kati yake na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Jenista Mhagama.
Akichangia Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu 2015/16, Lissu alisema Serikali hiyo imeshindwa karibu kila jambo, ikiwamo uandikishaji wa wananchi katika Daftari la Kudumu la Wapigakura.
Alisema uchovu huo pia umejidhihirisha wazi baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kueleza kwamba mpaka sasa haijapewa fedha za maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, wakati imebaki miezi mitano ufanyike.
Lissu alivutana na Spika Anne Makinda pale alipotakiwa kukaa chini kumpisha Mhagama azungumze baada ya kugoma kwa maelezo kuwa waziri huyo ameingilia wakati akitoa ufafanuzi wa uchovu wa Serikali.
Mvutano huo ulianza Lissu alipokuwa akisema kuwa mbali na kukwama kwa uandikishaji katika Daftari la Wapigakura, hata katika upigaji wa kura za kupitisha Katiba Inayopendekezwa katika Bunge Maalumu la Katiba, marehemu, mahujaji na wagonjwa ni miongoni mwa wajumbe wa Bunge hilo waliopiga kura.
"Hata Uchaguzi Mkuu mpaka sasa Serikali haijatoa fedha kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, hakuna maandalizi yoyote. Hatukubali kuona Serikali hii ikijiongezea muda kwa kisingizio hicho," alisema Lissu.
Kauli hiyo ilimwinua Mhagama na kueleza kuwa katika Bunge la Katiba zilipigwa kura halali, huku akifafanua jinsi Serikali ilivyofanya shughuli nyingi za maendeleo.
"Mheshimiwa Spika, Lissu analidanganya Bunge. Kauli zake ni za kuudhi namwomba asiendee kupotosha umma," alisema Mhagama huku Lissu akisisitiza kauli yake.
Wakati Mhagama akisimama kuomba utaratibu wa Spika, Lissu naye alisimama akipinga kitengo cha kukatizwa na waziri huyo kuchangia, tukio ambalo liliingiliwa na Spika na kuzua majibizano.
"Huyu ananizuia kwa misingi gani, kafuata utaratibu upi," alisema Lissu huku Mgahama naye akiendelea kuzungumza huu akiwa amesimama kabla ya wote wawili kukatishwa na Spika Makinda aliyewataka wakae chini na kufafanua kuwa yeye ndiye anayejua utaratibu.
Baada ya kutoa ufafanuzi huo, Makinda alimpa nafasi Mhagama kuendelea kuzungumza na alipomaliza alimpa nafasi Lissu ili amalizie kuchangia hotuba hiyo.CHANZO: MWANANCHI (Muro)

No comments:

Post a Comment