TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, May 13, 2015

Mtu mmoja auawa katika machafuko mapya Bujumbura

Ofisi mbili za chama tawala zabomolewa, baada ya mtu mmoja kuuawa kwa kupigwa risasi na polisi. Gari ya mkuu wa Wilaya ya Buterere imechomwa moto, Mei 12 mwaka 2015.
Na RFI
Hali ya usalama imeendelea kudoroara nchini Burundi, hasa katika mji wa Bujumbura. Raia mjini humo wameendelea kushikilia msimamo wao wa kuandamana hadi rais Pierre Nkurunziza atakapo achana na mpango wake wa kuwania muhula wa tatu.
Maandamano yameingia Jumanne Mei 12 katika siku yake ya kumi na tano mjini Bujumbura, ambapo wanawake na wasichana wameonekana katika mstari wa mbele katika maadamano hayo.
Zaidi ya wanawake na wasichana wameandamana katika wilaya ya Musaga, kusini mwa jiji la Biujumbura. Maandamano hayo ya wanawake na wasichana yamefanyika siku mbili baada ya maandamano mengine ya wanawake na wasichana wasomi yaliyofanyika mjini kati Bujumbura Jumapili mwishoni mwa juma hili lililopita.(P.T)
Wanawake na wasichana wa wilayani Musaga wameapa kuendelea na maadamano. Uamzi huo wa wanawake na wasichana wa kuandamana umekaribishwa na waandamanaji walioanza maandamano hayo.
Mtu mmoja aauawa kwa kupigwa risasi wilayani Buterere
Wilayani Buterere, kaskazini magharibi mwa jiji la Bujumbura, maandamano yameendelea. Katika maandamano hayo wameonekana pia wanawake na wasichana. Wakati huo huo polisi ilijitahidi kuwatawanya waandamanaji. Mtu mmoja ameuawa kwa kupigwa risasi na askari polisi mapema Jumanne asubuhi wiki hii.
Kutokana na hali hiyo waandamanaji wamepandwa na ghadhabu na kuamua kuchoma moto ofisi mbili za chama tawala cha Cndd-Fdd, na baadaye walijaribu kushambulia nyumba ya afisa wa polisi anayejulikana kwa jina maarufu Ayubu, ambaye amekua akituhumiwa na waandamanaji kuwa amekua akijihusisha na vitendo vya kikatili dhidi ya waandamanaji. Wakati huo huo gari ndogo la mkuu wa wilaya ya Buterere limechomwa moto na waandamanaji wenye hasira.
Duru kutoka shirika la msalaba mwekundu, zaidi ya watu 150 wamejeruhiwa kataika maandamano hayo, na wamelazwa katika hospitali mbalimbali za mji wa Bujumbura.
Hayo yanajiri wakati viongozi mbalimbali kutoka Umoja wa Afrika wakiwemo marais wa nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika ya Kati wakitazamiwa kukutana jijini Dar es Salaam kwa minajili ya kutafutia suluhu machafuko yanayoendelea nchini Burundi.
Rais Nkurunziza ameendelea na msimamo wake wa kuwania muhula wa tatu, baada ya viongozi mbalimbali ikiwa ni pamoja na Umoja wa Mataifa, Umoja wa Ulaya, Umoja wa Afrika, Marekani na mataifa jirani kumnasihi rais huyo kujiondoa katika kinyanga'nyiro hicho cha kuwania urais.

No comments:

Post a Comment