TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, May 15, 2015

MARAIS AFRIKA MASHARIKI WALAANI JARIBIO LA KUPINDULIWA NKURUNZINZA 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akizungumza na waandishi wa habari mapema leo asubuhi kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu J.K. Nyerere, jijini Dar es salaam.
Na Chalila Kibuda
MARAIS wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wamelaani kitendo cha baadhi ya askari kufanya jaribio la kutaka kuipindua serikali ya Burundi.
Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es salaam leo, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe amesema kuwa hali ya Burundi ni tete na kwamba japo linaonekana ni jambo dogo lakini linaweza kugharimu maisha ya watu.
"Hivyo tunatakiwa tuvute subira...Tusubiri na sio kulitangaza suala hilo kiushabiki wakati wenzetu wana tatizo. Afrika haitaki tena mtu yeyote kwa sababu yeyote kuhalalisha kuchukua nchi kwa mtutu", amesema Membe.
Amesema Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambalo lilikuwa na mkutano juzi na jana, litakaa tena wiki ijayo kujadili ajili ya hali ya Burundi.
Membe amesema, Wakuu hao wataketi tena Jumatatu baada ya kupata tathimini na watatoa taarifa ya kinachoendelea nchini Burundi, hivyo kwa sasa hawatazungumzia lolote.
Membe amesema kuwa hajui aliko Rais Pierre Nkurunzinza ambaye anadaiwa aliondoka nchini jana kurudi Burundi huku kukiwa na taarifa za kutokwepo kwa Rais huyo katika nchi yake kufuatia jaribio la kupinduliwa na baadhi wa askari wa nchi hiyo.(Muro)

No comments:

Post a Comment