TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, May 19, 2015

EU kupambana na wahamiaji haramu 

Wahamiaji wakiwa wameketi katika kituo kimoja mjini Tripoli wakiwa na matumaini ya kufika Ulaya
Umoja wa ulaya umekubali kuanzisha kikosi cha Jeshi la wanamaji kwa ajili ya kupambana na wafanya biashara wanaosafirisha watu kutoka Libya.
Mkuu wa sera za mambo ya kigeni wa EU,Federica Mogherini, amesema nia ni kuvunja mtandao unaowasafirisha wahamiaji kupitia bahari ya Mediterania.
Mogherini amesema umoja wa ulaya utaendelea kutafuta kuungwa mkono na Umoja wa Mataifa kuhusu kikosi hicho kipya.
Lakini Serikali ya Libya inayotambulika na jumuia ya kimataifa imesisitiza kuwa itahitaji kushirikishwa katika kuratibu operesheni za kijeshi dhidi ya wahalifu hao.
Balozi wa Libya ndani ya Umoja wa Mataifa, Ibrahim Dabbashi, amesema Mamlaka za libya hazijaelezwa chochote kuhusu Operesheni hiyo kwenye milki yake.
Dabbash amesema mipango ya EU pekee haiwezi kumaliza tatizo la wahamiaji haramu isipokuwa jamii ya kimataifa inapaswa kuisaidia Serikali halali ya Libya kuweza kudhibiti mipaka yake hali itakayorahisisha kukomesha wimbi la wahamiaji haramu.CHANZO:BBC (Muro)

No comments:

Post a Comment