TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, May 18, 2015

MKUU WA MKOA WA NJOMBE AFUNGUA KIKAO KAZI CHA BIASHARA YA KILIMO

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mh. Dk. Rehema Nchimbi akifungua kikao kazi cha biashara ya kilimo kwa kongani ya Ihemi iliyoandaliwa na SAGCOT (Southern Agricultural Growth Corridor of Tanzania) kwa ushirikiano na UONGOZI Institute (Taasisi ya Uongozi Afrika kwa Maendeleo Endelevu) mapema leo Iringa mjini. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Kilimo wa TCCIA Bi. Magadalena Mkocha, Mwenyikiti wa Bodi ya Agricultural Council of Tanzania Dk. Sinare Y. Sinare, DC wa Iringa Mh. Angeline Mabula, DC wa Mufindi Mh. Mboni Mhita na Katibu Mkuu Kiongozi mstaafu Philemon Luhanjo.
Katibu Mkuu Kiongozi mstaafu, Philemon Luhanjo ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa bodi ya UONGOZI Institute akitoa salaam kwa niaba ya taasisi hiyo wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha biashara ya kilimo kwa kongani ya Ihemi inayoendelea Iringa mjini. UONGOZI Institute imeshiriki katika kuwezesha kikao kazi hicho.
Mkurugenzi Mtendaji wa SAGCOT, Bw. Geoffrey Kirenga akitoa utangulizi wa mada ya biashara ya kilimo kwa nyanda za juu kusini. Mkutano huu wa siku mbili unakutanisha viongozi wa serikalini, sekta binafsi, mashirika ya kimataifa pamoja na wakulima kwa ajili ya kujadili kuhusu kuboresha biashara ya kilimo nchini kwa nyanda za juu kusini.
Picha ya pamoja ya wageni waalikwa na washiriki wa kikao kazi cha biashara ya kilimo inayoendelea Iringa mjini. Mada zinazojadiliwa ni pamoja na wajibu wa viongozi katika kuleta mageuzi katika kilimo.(Muro)

No comments:

Post a Comment