TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, November 5, 2012

UHABA WA NISHATI YA MAFUTA WALETA GUMZO BUNGENI
Mbunge wa Ubungo John Mnyika akiwasilisha hoja inayohusu  uhaba wa mafuta Bungeni
























Waziri Mkuu Mizengo Pinda (aliyesimama) akijibu hoja ya Mh. John Mnyika.
 
Na Mwandishi wetu, Dodoma.
 
Mbunge wa Ubungo (CHADEMA) John Mnyika akihoji kiti cha spika juu ya serikali kushindwa kuleta bungeni kauli ya serikali juu ya mkakati wa serikali kukabiliana na uhaba wa mafuta nchini Tanzania.
Uhaba wa mafuta leo umewakimbiza kwenye kikao cha bunge mjini Dodoma asubuhi, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na naibu mawaziri wake George Simbachawene na Steven Masele.
Waziri huyo na naibu mawaziri wake hawakuwepo bungeni leo wakati Mbunge wa Ubungo (CHADEMA) John Mnyika alitaka serikali itoe sababu ya kutokuja bungeni leo kutoa tamko la serikali ya jinsi inavyoshughulikia swala la uhaba wa mafuta nchini.
Spika wa Bunge Anne Makinda alimlazimisha Waziri kuu Mizengo Pinda kusimama na kujibu hoja ya Mnyika aliyemtaka Spika kulazimisha serikali ijibu hoja  yake pamoja na mkakati wa serikali wa kutatua uhaba wa mafuta nchini.
Waziri Mkuu  Mizengo Pinda alilazimika kunyanyuka nakusema kwa ufupi kuwa serikali ilikuwa ikijiandaa na kuja na hoja nzito ya kueleza umma mikakati kabambe ya kutatua uhaba wa mafuta nchini.

No comments:

Post a Comment