MALAWI KURUHUSU NDOA ZA JINSIA MOJA !
Serikali ya Malawi imesitisha 
rasmi mswaada wa sheria ya kupinga mapenzi ya jinsia moja na polisi 
wameagizwa kutowakamata watu wanaojihusisha na vitendo vya ushoga mpaka 
uamuzi mwingine utakapotolewa.
Mapenzi ya jinsia moja kwenye 
nchi ya Malawi yalipigwa marufuku na kutolewa kifungo cha miaka 14 jela 
kwa wanaokamatwa kushiriki na siku kadhaa zilizopita baadhi ya viongozi 
wa kimagharibi wametishia kusitisha kuzipa msaada nchi za Afrika ambazo 
zinakataa kutambua haki za mashoga.
Mmoja wa viongozi wa kijamii 
mwenye ushawishi mkubwa anaeitwa Kaomba, amiomba serikali kutoruhusu 
bunge kubadili sheria zake kuhusu ushoga huku akisema ni kinyume na 
maadili.
BBC Swahili wamesema mwandishi wao ambae yuko Blantyre anasema kuwa kusitisha kwa muda sheria hiyo, kutawaudhi sana watu wengi hasa viongozi wa kidini pamoja.
BBC Swahili wamesema mwandishi wao ambae yuko Blantyre anasema kuwa kusitisha kwa muda sheria hiyo, kutawaudhi sana watu wengi hasa viongozi wa kidini pamoja.
Kama unakumbuka… mwaka 2010 
wanaume wawili walikamatwa na kushtakiwa kwa utovu wa nidhamu hadharani 
baada ya kusema wataoana ambapo hiyo kesi ilikua kero kwa mataifa 
yanayosupport hizo ndoa za jinsia moja na hata kusababisha baadhi yao 
kusitisha msaada kwa Malawi, na ikawa pigo kubwa kwa nchi hiyo ambayo ni
 moja ya nchi maskini zaidi duniani.
Rais wakati huo akiwa Bingu wa 
Mutharika aliwasamehe wanaume hao kwa misingi ya kibininadamu ingawa 
alisisitiza kuwa ni kinyume na maadili ,na hata tamaduni za kiafrika na 
sheria za nchi.
Hata hivyo rais Joyce Banda aliyemrithi Bingu amewaambia wabunge kwamba anataka kubatilisha sheria hiyo na kuhalalisha mapenzi ya jinsia moja.
Hata hivyo rais Joyce Banda aliyemrithi Bingu amewaambia wabunge kwamba anataka kubatilisha sheria hiyo na kuhalalisha mapenzi ya jinsia moja.

No comments:
Post a Comment