TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, November 7, 2012

ILICHOKISEMA TFF NA SIMBA KUHUSU GOLIKIPA KASEJA
Katibu Mkuu wa Shirikisho Angettile Osiah





























Uongozi wa Shirikisho la soka nchini TFF umeungana na uongozi wa klabu ya simba kwa kuwataka baadhi ya mashabiki na wanachama wa klabu hiyo kuonyesha heshima dhidi ya kipa Juma Kasseja na sio kumchukulia kama mtu wa kawaida.
Katibu mkuu wa TFF Angetille Osiah amesema wamesikitishwa na tuhuma za wanachama na mashabiki wa klabu ya simba ambazo zimeelekezwa kwa kipa huyo baada ya club yake kufungwa 2- 0 na Mtibwa  Morogoro.
Baadhi ya mashabiki wa Simba walioandamana mpaka kwenye makao makuu ya Club hiyo walisema kipa huyo ambae wanadai kiwango chake kimeshuka, anazo tuhuma pia kwamba anapokea rushwa ili kuachia magoli.
Namkariri Angetille akisema “nimesikitishwa na baadhi ya maneno ambayo anashutumiwa kipa Kaseja, kwa kweli inasikitisha kwa kipa kama yule ambae ameitumikia Simba kwa muda mrefu ameiletea mafanikio makubwa, kumrushia maneno mabaya ambayo kwa kweli yatamkatisha tamaa, ameitumikia Simba kwa uaminifu kwa muda mrefu sana na hata juzi walipokua wanaulizia kwamba  ana kadi ngapi za njano na sisi tulikua tunasikitika kwamba jamani mchezaji amechoka na yeye anacheza kila mechi, wakati mwingine anaweza kukosea kwa sababu ya uchovu, kila mechi anacheza yeye timu ya taifa inamtegemea yeye, tusije tukamshutumu kwa makosa ambayo pengine yangeweza kuzuilika kama angekua anaweza kupumzishwa na yeye”

No comments:

Post a Comment