ILICHOKISEMA TFF NA SIMBA KUHUSU GOLIKIPA KASEJA
![]()  | 
| Katibu Mkuu wa Shirikisho Angettile Osiah | 
Uongozi wa Shirikisho la soka 
nchini TFF umeungana na uongozi wa klabu ya simba kwa kuwataka baadhi ya
 mashabiki na wanachama wa klabu hiyo kuonyesha heshima dhidi ya kipa 
Juma Kasseja na sio kumchukulia kama mtu wa kawaida.
Katibu mkuu wa TFF Angetille 
Osiah amesema wamesikitishwa na tuhuma za wanachama na mashabiki wa 
klabu ya simba ambazo zimeelekezwa kwa kipa huyo baada ya club yake 
kufungwa 2- 0 na Mtibwa  Morogoro.
Baadhi ya mashabiki wa Simba 
walioandamana mpaka kwenye makao makuu ya Club hiyo walisema kipa huyo 
ambae wanadai kiwango chake kimeshuka, anazo tuhuma pia kwamba anapokea 
rushwa ili kuachia magoli.
Namkariri Angetille akisema 
“nimesikitishwa na baadhi ya maneno ambayo anashutumiwa kipa Kaseja, kwa
 kweli inasikitisha kwa kipa kama yule ambae ameitumikia Simba kwa muda 
mrefu ameiletea mafanikio makubwa, kumrushia maneno mabaya ambayo kwa 
kweli yatamkatisha tamaa, ameitumikia Simba kwa uaminifu kwa muda mrefu 
sana na hata juzi walipokua wanaulizia kwamba  ana kadi ngapi za njano 
na sisi tulikua tunasikitika kwamba jamani mchezaji amechoka na yeye 
anacheza kila mechi, wakati mwingine anaweza kukosea kwa sababu ya 
uchovu, kila mechi anacheza yeye timu ya taifa inamtegemea yeye, tusije 
tukamshutumu kwa makosa ambayo pengine yangeweza kuzuilika kama angekua 
anaweza kupumzishwa na yeye”

No comments:
Post a Comment