TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, November 7, 2012

STORI KUHUSU YANGA KUOMBA RADHI























Uongozi wa klabu ya Yanga umeomba radhi kwa taarifa zilizotolewa novemba   kuhusu uteuzi wa meneja Shaban Katwila, Afisa Mawasiliano Baraka Kizuguto, habari ambazo zilitolewa na Kaimu Katibu Mkuu Lawrence Mwalusako.
kwenye website yao wameandika kwamba Mwalusako kasema anaomba radhi kwa hali iliyojitokeza kwa sababu ameharakisha kutangaza uteuzi huo ambao bado ulikua haujadhibitishwa.
Amekaririwa akisema “Mtu anapoteuliwa kushika nafasi ya kazi, inapaswa kumpa taarifa muhusika baada ya hapo mnakaa mwajiri na mwajiriwa kukubaliana mazingira ya utendaji kazi na taratibu nyingine, hiki kitu kilikua bado hakijafanyika hivyo kitakapokua tayari tutawajulisha tena”
Kikao cha kamati ya utendaji kilikaa mwishoni mwa wiki na kupendekeza Katwila na Kizuguto kushika nafasi hizo, lakini taratibu za ufanyaji kazi wao zilikuwa bado hazijajdiliwa, hivyo hayo ndo makosa yaliyofanyika kuwatangaza rasmi wakati bado makubaliano hayafikiwa.

No comments:

Post a Comment