TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, November 9, 2012

UFISADI WA MABILLION USWISI WATIKISA NCHI

Na Julius Magodi na Habel Chidawali, Dodoma

MJADALA mkali uliibuka bungeni jana baada ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema) kuwalipua baadhi ya viongozi waandamizi wa Serikali akitaka wachunguzwe kwa makosa ya kuficha mabilioni ya fedha nje ya nchi.
Zitto alitoa kauli hiyo jana bungeni wakati akiwasilisha hoja yake binafsi kuhusu kulitaka Bunge kuchunguza na kuielekeza Serikali kuchukua hatua dhidi ya raia wa Tanzania walioficha fedha na mali haramu nje ya nchi.
Bila ya kuwataja kwa majina, mbunge huyo aliwataja watu hao kwa nyadhifa kuwa ni watu wote walioshika nyadhifa za uwaziri mkuu katika kipindi cha 2003 hadi 2010, walioshika nyadhifa za uwaziri wa nishati na madini katika kipindi hicho na waliokuwa makatibu wakuu Wizara ya Nishati na Madini.
Wengine ni mawaziri na makatibu wakuu wa Wizara ya Ulinzi, wakuu wa majeshi, wanasheria wa Serikali, makamishna wa nishati, walioshika wadhifa wa Ukurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Uenyekiti na Ujumbe wa Bodi wa TPDC katika kipindi cha mwaka 2003 hadi 2010. Kutokana na hilo, Zitto aliitaka Serikali kupeleka bungeni muswada wa sheria bungeni wakati wa Mkutano wa 11 wa Bunge wa Aprili mwakani.
“Mbali na hilo napendekeza kuwa iwe ni marufuku kwa kiongozi yeyote wa umma au mume au mke wake au mtoto wake kuwa na akaunti nje ya nchi isipokuwa kwa sababu maalumu na kwa kibali rasmi kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano,” alisema Zitto.
Pia Zitto alitaka Serikali kuwasiliana na Benki ya Dunia kupitia kitengo cha ‘Assets Recovery Unit’ ili mabilioni ya fedha na mali ambazo zimetoroshwa nje ya nchi kwenda Uswisi, Dubai, Mauritus na maeneo mengine ziweze kurejeshwa.
Aliwataka Watanzania wote wenye akaunti za fedha nje ya nchi waeleze wamezipata wapi na Takukuru wachukue hatua za kisheria dhidi ya watu wote wanaomiliki fedha hizo kinyume cha sheria.
Zitto alisema katika mkutano wa Bunge la 11 na baada ya taarifa ya Kamati Teule ya Bunge kuhusu raia wa Tanzania wenye kumiliki fedha za kigeni kwenye benki na mali nje ya Tanzania ilete taarifa ya hatua ilizochukua ili kuziba mianya ya utoroshaji wa fedha nje ya nchi.
Alipendekeza kwamba Serikali katika bajeti ya mwaka 2013/14 ianzishe kodi maalumu ya asilimia 0.5 ya thamani ya fedha zilizotoroshwa ili kuweka rekodi za uhakiki fedha za ndani na zinazotoka nje.
Mbunge huyo alisema mazungumzo yake na wachunguzi wake binafsi kiwango cha fedha kinachomilikiwa na Watanzania Uswisi peke yake ni takriban mara 20 ya kiwango kilichotangazwa na benki ya taifa ya nchi hiyo. Alisema fedha hizo ni sehemu tu ya fedha ambazo Watanzania wamezificha katika benki mbalimbali za nje.
Alitoa mfano wa Benki ya UBS peke yake iliyopo katika nchi hiyo ina maofisa 240 ambao wanashughulikia wateja wa Tanzania na kila ofisa mmoja husimamia mteja mmoja mwenye kiwango kisichopungua dola za Marekani 10 milioni.
Zitto alisema Benki Kuu ya Uswisi ilitangaza kuwa jumla ya dola za Marekani 196 milioni zilikuwa zimehifadhiwa kwenye akaunti za benki za nchi hiyo. Alisema kuwa pamoja na Mkurugenzi wa Takukuru kukaririwa akisema kuwa ataiandikia Serikali ya Uswisi barua kuomba kurejeshwa kwa fedha hizo, lakini mpaka sasa hakuna hatua zilizochukuliwa.
CHANZO: MWANANCHI

No comments:

Post a Comment