TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, November 30, 2012

LEO SIKU YA UKIMWI DUNIANI  WAKAZI WA DAR WAHIMIZWA KUPIMA AFYA ZAO NA  JK KUHUTUBIA TAIFA
Mratibu wa Ukimwi wa Mkoa wa Dar es salaa kutoka TACAIDS Bw. Omary Chambo akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu hali ya maabukizi ya ugonjwa huo katika jiji la Dar es salaam na kutoa wito kwa wakazi wa jiji hilo kushirikiana na serikali na wadau mbalimbali katika kupambana na Ugonjwa huo
Na: Aron Msigwa MAELEZO. Dar es salaam.
Wakazi wa mkoa wa Dar es salaam wameshauriwa kujitokeza kupima afya zao mara kwa mara na kujiepusha na vitendo vinavyochangia maambukizi ya Virusi vya Ukimwi.
Akizungumza na waandishi wa habari kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Dar es salaam leo jijini Dar es salaam Afisa habari wa mkoa huo Bi. Adrofina Ndyeikiza amesema kuwa kuna umuhimu wa jamii kujitambua na kushiriki kikamilifu katika kufanya tathmini ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi na namna bora ya kujikinga.
Amesema kila mwaka ifikapo tarehe 1 Desemba Tanzania huungana na mataifa mengine kuadhimisha siku ya Ukimwi Duniani kwa kuwahusisha wadau mbalimbali ambao wote kwa pamoja hupata nafasi ya kutathmini mikakati ya kudhibiti Ukimwi iliyofanyika kwa muda wa mwaka mzima na kutafuta mbinu za kuboresha harakati hizo.
Amesema maadhimisho hayo yatakayofanyika katika viwanja vya Biafra jijini Dar es salaam umeichagua na kuipa heshima manispaa ya Kinondoni kuandaa maadhimisho hayo
“Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi duniani mwaka huu yanabeba ujumbe ule ule uliotolewa mwaka jana ambapo kauli mbiu hii inaendelea mpaka mwaka 2015 na kwa mwaka huu jijini Dar es salaam yanafanyika katika uwanja wa Biafra yakiongozwa na kauli mbiu ya Tanzania Bila Maambukizi Mapya, Unyanyapaa na vifo vitokanavyo na Ukimwi Inawezekana”
Amesema lengo la kauli mbiu hiyo ni kuhamasisha na kuelimisha zaidi jamii kuhusu VVU na Ukimwi na kubadilisha tabia ili kujikinga na maambukizi ya mapya ya VVU, kuhamasisha jamii kuacha kabisa unyanyapaa, unyanyasaji na ubaguzi kwa watu wanaoishi na VVU na ubaguzi kwa watu wanaoishi na VVU na UKIMWI na kuboresha huduma za afya na tiba ya magonjwa nyemelezi na dawa za kufubaza makali ya VVU (ARVs).
Bi. Ndyeikiza amesema kuwa mbali na maadhimisho hayo katika mkoa wa Dar es salaam serikali kwa kushirikiana na Asasi zisizo za kiserikali zilizo katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo zinaendelea kuwapatia wananchi huduma za elimu, ushauri na upimaji wa hiari wa VVU katika maeneo mbalimbali.
Kwa upande wake mratibu wa Ukimwi wa mkoa wa Dar es salaam kutoka Tume ya Kudhibiti Ukimwi nchini (TACAIDS) Bw. Omary Chambo amesema kuwa jamii bado inahitaji elimu juu ya namna na mikakati ya kukabiliana na virusi vya Ukimwi na hatimaye kupunguza maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi.
Amesema takwimu za mwaka 2012 kwa mkoa wa Dar es salaam zinaonyesha kuwa katika Manispaa ya Ilala hali ya maambukizi ni 8.3%, Temeke 6% na Manispaa ya Kinondoni ni 6.7 na kuongeza kuwa vitendo vya unyanyapaa miongoni mwa jamii kwa waathirika wa ugonjwa huo vinachangia watu wengi wasijitokeze kupima kwa hiari ili kujua kama wanaishi na VVU.
“Vitendo vya unyanyapaa vimekua sababu ya kuwafanya wengi wasijitokeze kupima kuhofia kutengwa na jamii pindi watakapogundulika kuwa wameathirika , hivyo tunaendelea na juhudi ya kuwaelimisha wananchi kuepuka vitendo hivyo na wajitokeze kupima afya zao kwa hiari” ameeleza Bw. Omary.

No comments:

Post a Comment