TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, November 15, 2012

LADY JAY DEE KUTOA SOMO KWA WASANII CHIPUKIZI
Mkuu wa vipindi vya East Africa TV Lidya Igabaruza na Lady Jay Dee
Muimbaji mahiri wa kike hapa nchini Judith Wambura (kulia) almaarufu kwa jina la Lady Jay Dee akizungumza na waandishi wa habari leo katika mgahawa wake wa ‘Nyumbani Lounge’ uliopo jijini Dar es Salaam na kutambulisha rasmi kipindi chake kipya cha luninga kitakachoitwa‘Diary ya Lady Jay Dee’.
Amesema madhumuni ya kipindi hicho ni kuleta burudani tofauti kwa wapenzi wa muziki wake na muziki wa kizazi kipya kwa ujumla, vilevile kitatoa fundisho na changamoto kwa wasanii chipukizi kujua wasanii wakongwe wamepitia katika vikwazo gani.
Lady Jay Dee amesema kipindi hicho kitaonyeshwa ndani ya East Africa Television kuanzia tarehe 18 Novemba mwaka huu kila siku ya Jumapili.
Aidha ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa makampuni mbalimbali kujitokeza kushiriki katika kudhamini vipindi vinavyobuniwa kama hivyo ili kuweza kutoa ajira kwa wasanii na wadau wengine wa sekta ya muziki na burudani.

No comments:

Post a Comment