MAHAKAMA YAAMURU MADIWANI WATANO KUILIPA CHADEMA SH. MILLION 15
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Arusha, imewaamuru madiwani watano waliotimuliwa Chadema kulipa gharama za kesi waliyokuwa wamefungua kupinga kufukuzwa uanachama, vinginevyo watapelekwa magereza.
Hakimu
 Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Charles Magesa alitoa hukumu hiyo jana
 baada ya Chadema kushinda kesi hiyo.Hakimu Magesa alisema madiwani hao 
wanapaswa kulipa Sh15 milioni ndani ya miezi miwili, wakishindwa 
watapelekwa gerezani.
Madiwani hao ni Estomih Mallah (aliyekuwa Naibu 
Meya ya Manispaa ya Arusha kipindi hicho), John Bayo aliyekuwa Diwani wa
 Elerai, Reuben Ngowi (Themi), Charles Mpanda (Kaloleni) na Rehema 
Mohamed aliyekuwa Diwani wa Viti Maalumu.
                
              
Pia, katika kesi hiyo ya madai Chadema walikuwa 
wakiwakilishwa na Wakili Method Kimomogoro, wakati wadaiwa hao walikuwa 
wakijitetea wenyewe baada ya aliyekuwa wakili wao kujitoa.Akisoma uamuzi huo, Hakimu Magesa alisema baada ya
 mahakama kupitia hoja za pande zote, imeona wadaiwa hao wanapaswa 
kulipa zaidi ya Sh15.1 milioni, kila mmoja anatakiwa kulipa zaidi ya 
Sh3.2 milioni katika kipindi kisichozidi miezi miwili.
Awali, kulikuwa na mvutano kati ya wadaiwa hao 
jambo lililosababisha kesi hiyo kusikilizwa kwa kipindi kirefu ambapo 
walitakiwa kueleza mahakama hiyo sababu ya kutokupelekwa gerezani, huku 
kila mmoja akitamka kiwango cha fedha ambacho angeweza kulipa kwa mwezi.
                
              
Kwa upande wake, Ngowi alisema ana uwezo wa kulipa
 Sh25,000 kwa mwezi, Mpanda Sh20,000, Mallah Sh20,000, Rehema Sh15,000 
na Bayo Sh15,000 kwa mwezi bila kuonyesha mchanganuo wa kipato chao, 
jambo lililopingwa vikali na Wakili Kimomogoro kwamba kiwango hicho ni 
kidogo.
                
              
Hakimu Magesa alisema kisheria mtu akishinda kesi 
ana uwezo wa kuchagua hukumu ya kulipwa kwa kuchukua mali za mdaiwa au 
mlalamikiwa kupelekwa kifungoni.
                
              
“Kimsingi mtu anaposhinda kesi lazima alipwe 
gharama aliyotumia na iwapo mahakama itaridhia alipwe kwa kiwango hicho,
 itachukua muda mrefu kati ya miaka 10 na 16 kumaliza deni hilo, jambo 
litakalosababisha aliyeshinda kushindwa kuona matunda ya ushindi wake,” 
alisema Magesa.
                
              
Alisema fedha hizo wanapaswa kuzilipa mara mbili, 
 awamu ya kwanza inatakiwa kila mmoja kulipa zaidi ya Sh1.5 milioni na  
wawe wamemaliza kwa miezi miwili na kwamba, iwapo watashindwa mdai 
anaweza kupeleka mchanganuo wa gharama za kumtunza mfungwa na mahakama 
kuupitia na baadaye kutoa amri wapelekwe 
gerezani

No comments:
Post a Comment