TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, February 14, 2013

WAWEKEZAJI WATAKIWA KUWEKEZA ARUSHA
Mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo akiwa anakata utepe wa lango la kuingia katika ukumbi wa World Garden uliozinduliwa leo jijini Arusha

























Na: Woinde Shizza ,Arusha
Mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo amewataka wananchi wa mkoa wa Arusha kuanza kuwekeza katika sekta mbalimbali ili kuweza kuweka mkoa huo katika madhari  na hadhi ya jiji. Aliyasema hayo jana wakati akifungua jengo jipya la mikutano pamoja na ukumbi wa disco lililopo jijini hapa lijulikanalo kwa jina la World garden lililopo katika kata ya
mshono ndani ya jiji la Arusha
Alisema kuwa   mkoa wa Arusha kwa sasa umepandishwa hadhi na kuwa jiji hivyo ni wajibu wa wazawa kuwekeza katika mambo mbalimbali  akitolea mfano kuwa mpaka sasa pamoja ya kuwa   wananchi ni wengi na wageni ni wengi lakini mpaka sasa kuna sehemu super makerti moja tu kitu ambacho kinatia aibu kwa jiji kubwa kama hili
Alisema kuwa viwanja vipo vya kujengea sehemu hizo ni watu wa kuwekeza tu hivyo aliwasihi wawekezaji wajitokeze kwa wingi kuwekeza katika vitu mbalimbali ili kuweza kuwezesha jiji letu kuwa la kimataifa
Alibainisha kuwa wafanyabiashara wakubwa wamekuwa wanaogopa kwenda kuchukumikopo na kuwekeza katika vitu mbalimbali lakini aliwatoa hofu na kuwaambia kuwa mikopo ipo na ni haki ya kila mmoja kwenda kuchukuwa mkopo kwani nafasi zipo wazi na mikopo ipo ya kutosha huku akibainisha kuwa amna mfanyabishara yeyote mkubwa anafanya kitu pasipo kuchukuwa mkopo
Alipongeza uongozi wa kampuni ya World Garden na kudai kuwa wameweza kupiga atua kubwa kwani kufungua kwao kwa jengo hilo litasaidia kwa kiasi kikubwa kwani vijana wengi watapata ajira kupitia jengo hilo kwani katika jengo hilo kuna vitu vingi kwama vile ukumbi wa disco watu wa usafi wa nje na mengine mengi ambapo watu wote wanaotakiw akufanya kazi huku  ni watanzania vijana hivyo watakuwa wamesaidia vijana kupata ajira
 Kwa upande wake  mkurugenzi mtendaji wa World Garden alisema kuwa wao kama kampuni yao inampango wa kutoa ajira kwa zaidi ya vijana 120 na pia alisema kuwa watajitaidi kuboresha vitu mbalimbali .

No comments:

Post a Comment