BABA MTAKATIFU AANZA WIKI YA KUFUNGA NA KUTOONEKANA HADHARANI

Baba
 Mtakatifu Benedict wa 16 ameanza wiki yake ya mafungo ya kiroho ambapo 
atakuwa haonekani hadharani kwa wiki nzima ikiwa ni mwanzo wa safari 
yake ya kuelekea kuachia rasmi uongozi wa kanisa Katoliki na kusema kuwa
 ana matumaini ibada zake zitakuwa na mafanikio.
 Baba
 mtakatatifu atabakia Vatican na baadhi ya wasaidizi wake wa karibu kwa 
ajili ya ibada za awali za sikukuu ya Pasaka na atapata mapumziko mafupi
 kila siku kwa ajili ya kuonana na katibu wake Georg Gaenswein, ili 
kuyashughulikia masuala ya dharura ya kanisa.
 Baada
 ya wiki nzima ya ibada, Baba Mtakatifu atakutana na rais wa Italia, 
Giorgio Napolitano, tarehe 23 Februari kushiriki ibada ya Jumapili yake 
ya mwisho ifikapo tarehe 24 mwezi huu na kuzungumza hadharani kwa mara 
ya mwisho mbele ya waumini wapatao 10,000.
Kiongozi
 huyo wa kanisa Katoliki duniani ataachia uongozi rasmi tarehe 28 mwezi 
huu na inasemakana kuwa Waziri wa Utamaduni wa Vatican Kadinali 
Gianfranco Ravasi ndiye anayeonekana mtu mwenye nafasi kubwa ya kuchukua
 nafasi yake kwa muda mfupi au mrefu.
No comments:
Post a Comment