TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, February 13, 2013

BUNGE LA UFARANSA LAIDHINISHA NDOA ZA JINSIA MOJA NA KUASILI WATOTO





















Bunge la Ufaransa limeupitisha mswada unaoruhusu watu wa jinsia moja kuoana na pia kuwa na haki ya kuasili watoto.
Wabunge wa chama cha Kisoshalisti cha rais Francois Hollande, wameupitisha mswada huo kupitia kikao cha bunge.

Hatua hii inaifanya Ufaransa kujiunga na orodha ya nchi nyingine duaniani, nyingi zikiwa za Ulaya ambazo zinaruhusu ndoa za jinsia moja na kuasili watoto kwa wanandoa hao.
 
 Hatua hiyo, imekuja baada ya maandamano makubwa katika wiki za hivi karibuni yaliyokuwa yakipinga mswada huo uliopewa jina la “ndoa kwa wote”. 
Uchunguzi wa maoni unaonyesha kuwa Wafaransa wengi wanaunga mkono ndoa za jinsia moja.

No comments:

Post a Comment