MWAIKIBAKI ATEMBELEA KIWANDA CHA MAGEREZA
 Rais wa 
Kenya, Mwai Kibaki (kushoto) akimsalimia Mkuu wa Jeshi la Magareza 
nchini, Kamishna Jenerali John Minja kabla ya kuingia ndani ya  Kiwanda 
cha Magereza Ukonga, jijini Dar es Salaam. Wa pili kutoka kushoto ni 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi, anayefuata ni 
Naibu Waziri wa wizara hiyo, Pereira Ame Silima.
Rais wa 
Kenya, Mwai Kibaki (wapili kutoka kulia) akiwa na Waziri wa Mambo ya 
Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (wa pili kutoka kushoto),  Mkuu wa 
Magereza nchini, Kamishna Jenerali John Minja (kulia) pamoja na maofisa 
mbalimbali kutoka nchini na Kenya, wakiingia ndani ya kiwanda hicho.
Mshauri 
Mtaalamu wa Mradi wa Kiwanda cha kutengeneza kofia ngumu katika Jeshi la
 Magereza, Alpherio Moris (kulia) akimuonyesha Rais Mwai Kibaki moja ya 
kofia ngumu (Helmet) ambayo inatarajiwa kutengenezwa na kiwanda cha 
magereza Ukonga hivi karibuni.
 Mkuu wa Jeshi la Magereza, Kamishna Jeneral John Minja (kushoto) akimkabidhi zawadi maalum ya kiti Rais Mwai Kibaki wa Kenya.
Rais Mwai 
Kibaki (wa kwanza kutoka kulia aliyevaa tai) akiwafurahia Askari 
Magereza na ofisa kutoka nchini Kenya wakiwa wamekaa kwenye kiti cha 
wapendanao kilichotengenezwa na wafungwa kiwandani humo.
 Rais Mwai
 Kibaki (wa pili kushoto) akiwa na maofisa mbalimbali wakiondoka Kiwanda
 cha Magereza Ukonga baada ya kumaliza kuangalia vifaa mbalimbali 
vinavyotengenezwa na kiwanda hicho.
Rais Mwai Kibaki akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali nchini pamoja na maofisa kutoka nchini Kenya.
PICHA ZOTE NA 
KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
No comments:
Post a Comment