TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, February 15, 2013

NEEC NA NDC WASAINI MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO WA KUWAWEZESHA KIUCHUMI






















Dk Anacleti Kashuliza Katibu Mtendaji wa  Baraza la Taifa La Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi  NCC akibadilishana mikataba wa ushirikiano kuwawezesha wananchi na Kaimu Mkurugenzi Mwendeshaji  wa Shirika la Maendeleo la Taifa NDC Bw. Shannel Mvungi           
Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) na Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) wameanzisha ushirikiano utakaowawezesha wananchi kiuchumi katika maeneo ambayo NDC imeanzisha miradi mbalimbali ya maendeleo. Manufaa haya kwa wananchi yanatokana na kusainiwa kwa Makubaliano ya ushirikiano kati ya mashirika haya ambao unalenga kutoa fursa kubwa za ushiriki wa kiuchumi kwa wananchi wa maeneo husika.Hadi sasa,
miradi inayolengwa ambayo inasimamiwa na NDC ni uchimbaji wa Makaa ya Mawe ya Mchuchuma na Chuma cha Liganga Wilayani Ludewa unaotekelezwa chini ya Kampuni ya ubia ya Tanzania China International Minerals Resources Limited ambao unatarajiwa kutoa ajira za moja kwa moja zaidi ya 5000 kwa watanzania ambazo ni fursa kubwa ya kukuza mapato ya wananchi wa  Ludewa.
 Matarajio ya NEEC na NDC ni kuwaendeleza na kuwawezesha kiuchumi wananchi walioko katika maeneo   ambayo miradi imeanza kutekelezwa ili waweze kujipanga na kujiandaa vema kufaidika na fursa hizo kwa kufanya yafuatayo:-
  1. Kutoa mafunzo ya ujengaji uwezo na ujuzi katika kutambua fursa zilizopo na jinsi ya kuzitumia,
  2. Kuhamasisha fursa na miundo mbinu ya kiuchumi,
  3. Kuhamasisha kujiunga katika Mitandao ya Vikundi na Masoko,
  4. Uwezeshwaji wa Upatikanaji wa Mitaji na kuunganishwa na Taasisi za Fedha,
  5. Kuainisha na Kuendeleza maeneo huru ya Kufanyia Biashara na
  6. Kuhamasisha Umuhimu wa Ushirika
 Lengo la makubaliano ya ushirikiano huu ni kuweka mifumo ya utekelezaji na usimamizi wa kuwaendeleza na kawawezesha wananchi katika maeneo ya miradi mbali mbali inayosimamiwa  na Shirika la Taifa la Maendeleo ili waweze kunufaika vema na rasimali asilia zinazowazunguka.
 Taasisi hizi mbili zinatarajia kushirikiana vema katika  kuwaunganisha wadau mbali mbali wa maendeleo katika maeneo husika hususani wawekezaji wa sekta binafsi,mashirika yasiyo ya kiserikali,wadau wa maendeleo na serikali za mikoa na wilaya katika kuwaendeleza na kuwawezesha wananchi katika maeneo husika.
 Ni matarajio ya Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) na Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) kuona rasilimali asilia zikiwanufaisha wananchi katika maeneo yao kwa kuwawezesha kushiriki kwa kiasi kikubwa katika shughuli za kiuchumi na kubadili hali zao za maisha kupitia ongezeko la kipato na kuboreka kwa miundombinu.
 Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) lilianzishwa chini ya kifungu cha nne (4) cha Sheria ya Taifa ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi . Baraza lilianza kazi rasmi mwaka 2005 likiwa ni chombo cha juu cha kusimamia utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi.
 Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC) ni chombo cha umma kinachomilikiwa asilimia 100 na Serikali, Shirika hilo lililoanzishwa mwaka 1965 kuchochea maendeleo ya nchi kupitia viwanda katika sekta zote za uchumi.

No comments:

Post a Comment