TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Sunday, February 24, 2013

JATA WAKABIDHI ZAWADI WANAFUNZI WALIOSHINDA INSHA ZENYE THAMANI YA DOLA ZA KIMAREKANI 800
Uongozi wa JATA wakipata picha ya pamoja na wanafunzi walioshinda isha katika hatua ya tatu bora ambao ni Maulid Juma mshindi wa pili kutoka shule ya Kibaha Sekondari, Faiza Khamis Ussi mshindi wa kwanza kutoka shule ya Sunni Madressa toka Zanzibar na Mshindi wa tatu ni Winfrida Leonard wa kidato cha tatu kutoka shule ya WamaNakayama
Uongozi huo ukipata picha ya pamoja na wanafunzi waliofanikiwa kuingia kumi bora katika shindano hilo ambao ni Faiza Khamis Ussi, Maulidi Juma, Winfrida Leonard , Halima Wingo III(Zahanaki) Charity Alphonce IV (Azania) Atupakisye I Kassanga III(WamaNakayama) Lucy Kamili III (WamaNakayama)Agness Kato IV (Zanaki) Asteria Ndalu IV (WamaNakayama) na Bill Brighton Laiderson I(Abbey)

Wanafunzi wakisikiliza kwa makini

Faiza akionyesha zawadi yake ya LapTop aina ya HP aliyokabidhiwa baada ya kushinda kuandika Isha kwa alama alizopata ni 81


Faiza na mwalimu wake akimsindikiza kupokea zawadi


 



Na Mwandishi wetu

SHIRIKA lilisilo la kiserikali toka Nchini Japan  JICA ALUMNI ASSOCIATION OF TANZANIA (JATA)  limetumia kiasi cha Dola 800 za Kimarekani  kutoa zawadi kwa wanafunzi wa shule za sekondali nchini  walioweza  kuandika  na kuisoma  insha iliyoandaliwa na  shirika hilo.

Mada ya isha hiyo ilikuwa inahusu Athari za Utandawazi  wa kisasa kwa vijana wa Tanzania ,ambapo jumla ya wanafunzi  31 walishiriki katika shule  sita zilizotoka Bara na Visiwani.

Katibu wa Shirika hilo Bi. Edina Ngerageza  alizitaja shule zilizoshiriki kuwa ni  Sunni Madressa , Kibaha , Wama Nakayama,Zahanaki , Abbey, Kibamba.

Bi. Ngerageza alisema lengo la shirikia hilo kuandaa isha hiyo ni kutaka kujua wanafunzi wanauwelewa gani kuhusu mambo ya Utandawazi  na jinsi inavyowaathiri vijana .

Alisema katika shindano hilo walimu waliwashirikisha wanafunzi wao , ambapo mambo mengi yalibainika kuhusu vijana kuelewa vizuri athari za utandawazi kwa jamii hii ya kizazi kipya kama matumizi ya Internet , simu na mambo mengine mengi.

Katika shindno hilo mwanafunzi Faiza Khanis Ussi wa kidato cha tatu kutoka shule ya Sunni Madressa toka Zanzibar  aliibuka kuwa mshindi wa kwanza kwa kupata alama 81  ambapo alizawadiwa Laptop moja aina HP na Certificate , mshindi wa pili ni Maulid Juma kidato cha tatu toka Kibaha secondary  alipata alama 77 alipatiwa music system  na mshindi wa tatu ni Winfrida Leonard  kidato cha tatu toka WamaNakayama  alipata alama 68 naye alipatiwa zawadi music system na wanafunzi wengine wote walipatiwa zawadi mbalimbali kwa wale walioshiriki zoezi hilo.

Akikabidhi zawadi hizo Afisa elimu wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Raymond Mapunda alisema JATA imetoa hamasa kubwa kwa vijana katika kuwapiwa uwezo wao juu ya uelewa wao katika utandawazi .

Alisema kama wanafunzi wakiwa makini kwa mambo ya utandawazi kwa kuepuka matumizi mabaya wanaweza kufanya vizuri katika masomo yao lakini kama wakitumia vibaya yatawasababishia madhara  makubwa.

No comments:

Post a Comment