TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, February 27, 2013

SERIKALI YA UGANDA YAJIPANGA KUWANUNULIA WABUNGE WAKE TOLEO IPYA LA IPAD ILI KUPUNGUZA GHARAMA ZA STESHENARI


Chama cha Forum for Democratic Change (FDC) kimepokea na kukubali mpango wa serikali ya Uganda wa kununua toleo jipya kabisa la iPads kwa ajili ya wabunge, lakini kimesema wabunge hao wakopeshwe na sio wapewe bure.
 
Msemaji wa Chama hicho Wafula Oguttu ambae pia ni mbunge, amesema pendekezo la kununua iPads halikataliwi lakini hakuna sababu ya kuwapa bure na badala yake wapewe kwa mkopo.
 
Serikali ya Uganda imepanga kununua iPads za kisasa na kuwapatia wabunge kwa lengo la kupunguza gharama ya steshenari.
 
Uamuzi huo ulichukuliwa hivi karibuni na Kamati ya Bunge na unasubiri utekelezaji kwa Kamati ya Mikataba.

No comments:

Post a Comment