LONDON FASHION WEEK TANZANIA IMO YA KUMI BORA

Nje ya 
Jumba la Somerset- Samson Soboye (Mpangaji wa maonyesho), Jacqueline 
Kibacha ("Heart 365"), Mama Balozi Joyce Kallaghe, Anna Lukindo ("Anna 
Luks") na Rose Kiondo (Mratibu wa maonyesho)

 Wanamitindo
 wa Kitanzania kwenye London Fashion Week 2013. Anna Lukindo, Christine 
Mhando, Jacquiline Kibacha-pic by Urban Pulse"
Jumapili 
mchana  wilaya ya Westminster jijini  London ilikuwa na mashindano ya 
ubunifu na urembo katika maonyesho  ya kimataifa ya London Fashion Week.
  Mashindano haya yalifanyika  jumba la Somerset lililosimama imara 
 kwenye upembe wa  kaskazi ya mto Thames.
 toka 
tarehe 14 hadi tarehe 28. Wiki hizi mbili nzima zitakutanisha kila mtu 
anaye husika na biashara ya mavazi na urembo. Magwiji na mapapa wa 
mitindo, wabunifu, walimbwende, watafuta vipaji, wafanya biashara, 
wazalishaji mali ghafi na wamiliki viwanda.  Wote hukutana katika 
maonyesho haya. Hapa si vipaji tu vinavyojionyesha, bali pia watu wa 
biashara.
Siku hii 
Tanzania ilikuwa moja ya nchi mbili tu za Kiafrika zilizochaguliwa na 
British Council na "London Fashion Week" kushiriki mashindano  ya 
kutafuta vipaji chipukizi kwenye tasnia ya ubunifu wa mavazi na urembo. 
 Watanzania Anna Lukindo, Jacqueline Kibacha na  Christine Mhando ndio 
wasanii waliobeba bendera ya taifa letu na kutuwakilisha katika 
mashindano haya ya kimataifa yanayofanyika kila mwaka kwa zaidi ya miaka
 27 sas
No comments:
Post a Comment