TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, March 30, 2015

Wakazi wa kata ya kidete wilayani kilosa,Morogoro wako hatarini kukubwa na mafuriko na njaa

Wakazi wa kata ya kidete wilayani kilosa, Morogoro wako hatarini kukumbwa na mafuriko na baa la njaa kufuatia kingo za bwawa kidete lililojengwa ili kuzuia maji yanayotiririka kutoka milimani na kuzua maafa ya mara kwa mara kwenye wilaya hiyo kupasuka na kuharibu maelfu ya hekari za mashamba huku pia hali hiyo ikitishia usalama wa reli ya kati ambayo ni kiungo kikubwa cha usafiri wa abiria na mizigo ndani na nje ya nchi.
Hofu ya kuzuka kwa mafuriko hasa kipindi hiki cha masika inaibuka kwa wakazi wa kata hiyo baada ya kingo za bwawa la kidete linalodaiwa kutafuna zaidi ya shilingi bilioni 3.5 kubomoka wakati ujenzi wake ukiendelea hali inayosababisha maji kutiririka kwa wingi na kuingia katika maeneo ua makazi na tayari yameshakwisha haribu maelfu ya hekari za mashamba na endapo mvua zitaendelea kunyesha kwa wingi maji hayo huenda yakaleta madhara kwenye reli ya kati amabayo inapita wilayani humo.
Mbali na kuzua hofu ya janga la mafuriko na baa la njaa kutokana na kuvunjika kwa bwawa hilo ambalo asili yake lilijengwa na wajerumani ili kuzuia maji yasiharibu miundombinu ya reli lakini pia lilikuwa likitoa ajira ya uvuvi kwa vijana ambao hapa wanaonyesha masikitiko yao ya kukosa kipato.
ITV inazungumza na mwenyekiti wa kijiji cha kidete stesheni yusuph bakari ambaye mradi wa bwawa hilo unatekelezwa katika eneo lake analalamikia siasa kuingizwa kwenye ujenzi wake ambao tayari umetafuna mabilioni ya fedha za walipakodi huku kukiwa hakuna dalili zozote za kukamilika kwa wakati. (CHANZO:ITV

No comments:

Post a Comment