TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, March 30, 2015

 DARAJA LA KIVULE DAR HATARINI KUKATIKA
 
Daraja linalolalamikiwa na wakazi wa eneo la Kivule jijini Dar.

Watembea kwa miguu pamoja na gari wakionekana kupita katika daraja hilo.

Mwonekano wa daraja hilo.
WATUMIAJI wa Barabara ya Kivule jijini Dar, wameilalalamikia serikali kwa kushindwa kutengeneza Daraja la Kerezange maarufu ‘Silali’ ambalo limekuwa kero kwa wakazi wa eneo hilo kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha ambazo zimesababisha daraja hilo kukaribia kukatika.(P.T)
Mwanahabari wetu alifanikiwa kuongea na baadhi ya raia wanaolitumia daraja hilo ambapo walisema kuwa kipindi hiki cha mvua maji huwa yanajaa mpaka juu ya daraja na kusababisha kushindwa kuvuka hali inayopelekea kukwamisha shughuli zao.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kivule-Ukonga, Waitara Mwita Mwikwabe, alisema kuwa tatizo la daraja hilo ni la muda mrefu kwani hata mwaka jana kuna tukio la mtu kufariki katika mto huo baada ya kutumbukia wakati maji yalipokuwa yamefunika daraja zima huku yeye akiwa anajaribu kuvuka.
Alisema kuwa Manispa ya Ilala inatambua tatizo hilo na iliwahi kupeleka mkandarasi kwa ajili ya kulitengeneza lakini cha kushangaza tangu alipoenda kulitazama hakurudi tena.
Alizidi kueleza kuwa, Halmashauri ya Wilaya ya Ilala ilisema katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2014/2015 chini ya Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli kuwa barabara ya eneo hilo pamoja na daraja hilo vingetengenezwa lakini mpaka sasa hakuna kilichofanyika.

No comments:

Post a Comment