TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, March 30, 2015

MT. MERU YAKABILIWA NA UPUNGUFU WA MASHUKA KUJIFUNIKIA WAGONJWA 

 Hospitali ya mkoa wa Arusha,Mt Meru inakabiliwa na upungufu mkubwa wa mashuka ya kujifunikia kwa ajili ya wagonjwa mbalimbali waliolazwa hospitalini hapo hali ambayo imepelekea baadhi ya wagonjwa hao kulala bila kujifunika nyakati za usiku.

Kwa sasa hospitali hiyo ina jumla ya vitanda 500 na mashuka 300 wakati wastani wa kitanda kimoja kinatakiwa kuwa na mashuka 8.
Akizungumza na waaandishi wa habari mara baada ya kupokea msaada wa jumla ya mashuka 100 na katoni kumi za maji kwa ajili ya wagonjwa waliolazwa hospitalini hapo,muuguzi mfawidhi wa hospitali hiyo,Sifael Masawe alisema kuwa tatizo la uhaba wa fedha kutoka serikali kuu limechangia kukosekana kwa huduma mbalimbali hospitalini hapo yakiwemo mashuka.
Alisema kuwa kwa nyakati tofauti baadhi ya wagonjwa hushindwa kujifunika mashuka nyakati za usiku kutokana na uhaba wa mashuka hayo na kuwataka wadau mbalimbali mkoani Arusha kujitokeza kuokoa hali hiyo.
Akikabidhi misaada ya mashuka na maji kwa ajili ya wagonjwa waliolazwa katika wodi wa akina mama hospitalini hapo ,mwenyekiti wa kikundi cha Upendo Family,Faustine Mwandago alisema kwamba misaada hiyo imegharimu kiasi cha zaidi ya sh,2 milioni.
Mwandago,alisema kuwa lengo la kukabidhi misaada hiyo ni kuonyesha upendo kwa watu wenye mahitaji mbalimbali sanjari na kulienzi jina la kikundi chao kwa vitendo huku akiwataka wadau wengine kuwaunga mkono.

No comments:

Post a Comment