TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, March 10, 2015

MTOTO WA MATUMLA KUMVAA MKOREA MACHI 27


Bondia mkongwe nchini Rashid Matumla, kutoka kushoto, Mohamed Matumla, Japhet Kaseba na Rais wa (TPBO), Yassin Abdallah 'Ustaadh' katika mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani).(P.T)

Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini Rais wa TPBO, Yassin Abdallah 'Ustaadh'.
BONDIA wa ngumi za kulipwa nchini Mohamed Matumla Jr ambaye ni mtoto wa gwiji wa zamani wa mchezo huo, Rashid Matumla ‘Snake Boy’ anatarajia kupanda ulingoni Machi 27, mwaka huu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee kugombania nafasi ya kwenda kushindania ubingwa WBF dhidi ya Mkorea, Wang Xi Hua.
Licha ya hivyo, Rais wa Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO), Yassin Abdallah ‘Ustaadh’, amewataja mabondia wengine watakaopanda ulingoni siku hiyo, wakati akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar, kuwa ni Japhet Kaseba atakayegombania ubingwa wa UBO Afrika dhidi ya Mada Maugo huku Thomas Mashali akitarajia kuwania ubingwa UBO  Afrika kilo 76 dhidi ya Karama Nyilawila.
 Picha/habari na Denis Mtima/ GPL

No comments:

Post a Comment