TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, March 24, 2015

Wabunge zaidi ya 10 watajiunga nami - Zitto

Aliekuwa Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),Zitto Kabwe akionyesha kadi ya Chama chake kipya yenye namba 007184 mbele ya waandishi wa habari waliofika kwenye mkutano wa Chama cha ACT-Tanzania,uliofanyika kwenye ukumbi wa Hoteli ya Serena,jijini Dar es Salaam
Akizungumza na gazeti la HabariLeo jana jijini Dar es Salaam, baada ya kuzungumza na waandishi wa habari, aLIYEKUWA Mbunge wa Kaskazini, Zitto Kabwe aliyejiunga rasmi na chama cha siasa cha ACT alisema nyuma yake wapo wabunge zaidi ya 10, watakaojiunga na ACT muda sio mrefu.(P.T)
"Siko mwenyewe wapo wenye mapenzi mema na tunataka kufungua ukurasa mpya kwa nchi yetu wa siasa za kujenga nchi, wabunge mahiri wa CCM na Chadema zaidi ya 10, watajiunga nami, ila sitakutajia majina kwa sasa kwa sababu ya sheria za vyama vyao, acha wamalizie vipindi vyao vya ubunge,"
alisema Zitto.
Zitto alisema amelipia ada ya miaka kumi ya uanachama wa chama hicho, ambayo kila mwaka ada ni Sh 1,000.
"Nimejiunga rasmi na ACT na nimelipa ada ya miaka 10 ya uanachama, nawakaribisha wote wenye mapenzi mema ya kujenga nchi wajiunge nasi", alisema Zitto. Majimbo 6 yanamsubiri.
Akizungumzia uchaguzi mkuu ujao, Zitto alisema atagombea nafasi ya ubunge kwa kuwa umri wake hauruhusu kugombea nafasi ya rais, na kwamba jimbo atakalogombea litawekwa wazi baada ya yeye kushauriana na washauri wake, kwa kuwa majimbo zaidi ya sita nchini yanamtaka agombee.
"Nitasema hapo baadaye ninagombea jimbo gani, kwa sababu majimbo mengi yananiita nikagombee; Kawe wananitaka, Segerea, Kasulu, Kahama, hivyo nitazungumza na wenzangu halafu nitasema nitagombea wapi"
alisema Zitto.
Alitetea uamuzi wake wa kuhamia ACT, akisema ni uamuzi sahihi kwa kuwa chama hicho kinaendana na kile alichokuwa anakipigania kwa miaka yote.

No comments:

Post a Comment