TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, March 25, 2013

WEMA SEPETU AFANYA KUFURU, BAADA YA KUMFANYIA MBWA WAKE SHOPPING YA MILLION 6, PIA AMEMTOA KAJALA JELA KWA SHILLING MILLION 13

KWA wale wenye hali ngumu kimaisha wataishia kusema; ni kufuru iliyoje kwani staa wa filamu za Kibongo, Wema Isaac Sepetu hivi karibuni amewafanyia mbwa wake wawili ‘shopping’ iliyogharimu dola 4,000 za Kimarekani (zaidi ya Sh. milioni 6.5 za madafu).
Sehemu ya shopping kwa mbwa wa Wema Sepetu.
Wema aliteketeza kiasi hicho cha fedha kwa kuwanunulia mbwa hao pafyumu, viatu na nguo, alivyoagiza kutoka nchini China, lengo likiwa ni kuhakikisha wanaishi katika mazingira mazuri.
Viatu kwa ajili ya mbwa wa Wema.
Akizungumzia ‘shopping’ hiyo nyumbani kwake Kijitonyama, jijini Dar, Wema alisema: “Kiukweli nawapenda sana hawa mbwa, ukinipasua roho yangu utawakuta ndiyo maana nataka wavae na kunukia vizuri, kinyume chake siwezi kuwa na amani.
Wema Sepetu.
“Najua watu wanaweza kushangazwa na kitendo cha mimi kutumia kiasi hicho cha fedha lakini sioni kama ni tatizo kwani ni kitu ambacho kinanipa furaha katika maisha yangu.”
 
Mmoja wa Mbwa wa Wema Sepetu.
Mbwa wa staa huyo aliowapa majina ya Van na Gucc wamekuwa ni gumzo kutokana na jinsi anavyowahudumia huku akiajiri watu maalumu wa kuhakikisha wanavaa, kula na kulala pazuri.


.
Mfuko wa pesa tasilim Sh. million 13 zilikwenda kuchukuliwa benki kwa ajili ya kumdhamini msanii mwenzao Kajala baada ya kuhukumiwa kwenda jela miaka 5 ama kulipa faini hiyo.
.
Wema akihojiwa na waandishi wa habari kuhusiana na tukio hilo
.
Kajala akiwa huru baada ya kukamilishwa kwa taratibu zote
Mungu amzidishie Wema kwa kile alichokitoa katika kufanikisha msanii mwenzake kuwa huru, ni jambo kubwa alilolifanya na anahitaji pongezi ,Ikiwa tutakuwa na moyo kama huo wote basi kila mmoja duniani angeishi kama mfalme

No comments:

Post a Comment