TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, March 12, 2013

WANAHABARI WATAKIWA KUFANYA UTAFITI WA KINA WANAPOANDIKA HABARI ZAO

Na Khadija Khamis –Maelezo Zanzibar
 Meneja wa Baraza la Habari kanda ya Zanzibar Suleiman Seif Omar ( Bin Seif) amewataka waandishi wa habari kufanya utafiti wa kina katika habari wanazoziandika kama zina ukweli na uhakika. Hayo aliyasema jana  wakati akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali katika ukumbi wa Mansoon Hotel Vuga Alisema
 waandishi wa habari wanapokuwa kazini wawe makini kuandika habari zinazozingatia maadili yote ya habari ikiwemo ukweli na uhakika.
 Alisema kuandika habari kwa kuzingatia vigezo hivyo kunamuwezesha mwandishi kuwa muadilifu na kujiamini katika kazi yake.
 Alisema Baraza la Habari Tanzania kazi yake ni kushajihisha waandishi wa habari na kuiwapa muongozo jinsi wa utafutaji wa habari na kuziandika  vyema ili ziwafikie wananchi wa  taifa hilo .
 “Kila mtu ana haki ya kupata habari ila habari hizo ziwe za ukweli na uhakika hivyo mwandishi nalazimika kuzifanyia utafiti wa kina habari anazozipata kabla ya kuziwasilisha kwa wananchi kupitia chombo cha habari”. Alisisitiza Bin Seif.
 Meneja huyo aliwaambia waandishi wa habari wawe watafiti wa habari na matukio ili kuziwasilisha kwa wananchi kama tukio hilo lilivyotokea.
 Nae mwandishi wa BBC Ali Saleh (Alibato ) alisema kuwa waandishi wa habari wanatakiwa kujifunza zaidi ili kuepukana na makosa ambayo hayastahiki kujitokeza na kuitia aibu fani hiyo.
 “Habari zipo lakini waandishi wa habari hakuna kutokazana na kutoweza kujifunza kusoma makala, vitabu pamoja kutosikiliza habari mbali mbali za ndani na nje ya nchi”. Alisema Ali Saleh.
 Nao waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo walisema hakuna uhuru wa kutosha katika kutoa habari jambo ambalo linawajengea hofu na kutokujiamini katika kazi zao .
 Mkutano huo wa  siku moja kwa  Waandishi wa Habari umeandaliwa na Baraza la Habari Tanzania  (MCT) ambao umebeba mada Haki ya Kupata Habari

No comments:

Post a Comment