TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, March 25, 2013

LIVE MATCH CENTRE: TANZANIA 3 - 1 MOROCCO


Dk 90+4 FULL TIME! TAIFA STARS 3-1 MOROCCO
Dk 90+3 Morocco inapata bao. TAIFA STARS 3-1 MOROCCO
Dk 90 Taifa Stars imefanya mabadiliko, ametoka Samatta ameingia John Bocco.
Dk 87 Ulimwengu anaumia baada ya kuangushwa na beki wa Morocco. Anatibiwa na kurudi uwanjani.
Dak 86: Taifa Stars 3-0 Morocco
Dk 80 RED CARD..! Achchakir Abderrahm wa Morocco anaonyeshwa kadi nyekundu baada ya kumtolea lugha chafu mwamuzi Helder Martins wa Angola.
Mbwana Samatta anaiandikia Tanzania bao la 3.
Dk 68 Morocco inafanya mabadiliko, ametoka Barrada Abdelaziz ameingia El Bahri Brahim.
Dk 67 GOOO....! Samatta anaifungia Taifa Stars bao la pili akimalizia mpira aliopenyezewa kutoka katikati ya uwanja baada mbio mabeki wa Morocco.
Dk 65 Yondani anavuruga vizuri mpira wa Eladoua Issam wa Morocco aliyekuwa anaenda kufunga.
Dak 63: Athuman Iddi anaingia kuchukua nafasi ya Mrisho Ngassa
Dk 61 Ngassa anachelewa kuunga krosi safi ya Samatta.
Dk 50 Taifa Stars inalishambulia zaidi lango la Morocco, uwepo wa Ulimwengu umeongeza kasi ya ushambuliaji ya Taifa Stars.
Dk 45 GOOO....! Thomas Ulimwengu anaifungia Taifa Stars bao la kwanza baada ya kuuwahi mpira ulioshindwa kuokolewa na mabeki wa Morocco na kufunga. TAIFA STARS 1-0 MOROCCO
Dk 45 Taifa Stars inafanya mabadiliko, ametoka Mwinyi Kazimoto ameingia Thomas Ulimwengu.
Dk 45 KIPINDI CHA PILI KIMEANZA!
Dk 45 HALF TIME! TAIFA STARS 0-0 MOROCCO.
Dk 45 Barrada Abdelaziz anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kumchezea vibaya Samatta.
Dk 41 Beki wa Taifa Stars, Kelvin Yondan amejitahidi kuharibu mipira mingi ya adui.
Dk 41 Beki wa Taifa Stars, Kelvin Yondan amejitahidi kuharibu mipira mingi ya adui.
Dk 38 Eladoua Issam wa Morocco anapiga kichwa chepesi kinachotoka nje kidogo ya lango la Taifa Stars.
Dak 35: Starz 0 - 0 Morocco
Dk 33 Beki wa Taifa Stars, Shomari Kapombe anaichambua ngome ya Morocco na kupiga shuti kali linalotoka nje ya lango.
Dk 31 Kaseja anadaka shuti kali la Achchakir Abderrahm.
Dk 25 Straika wa Taifa Stars, Mbwana Samatta anakosa bao la kichwa akiunga krosi ya Mrisho Ngassa.
Dk 24 Kipa wa Taifa Stars, Juma Kaseja anaokoa shuti kali lililoelekezwa langoni kwake.
Dk 18 Kiungo wa Taifa Stars, Salum Aboubakar 'Sure Boy' anapiga shuti kali kuelekea lango la Morocco lakini kipa Lamyaghri Nadir anaudaka mpira.
Dk 14 Beki wa Taifa Stars, Aggrey Morris anaukosa mpira kwa kichwa kuelekea lango la Morocco baada ya Taifa Stars kupata kona.
Dakika ya 9 timu zinashambuliana sana huku zikisomana.

Mpira umeanza hapanuwanja wa taifa.

Kikosi cha Taifa Stars kitakachoanza dhidi ya Morocco:1.Juma Kaseja2.Erasto Nyoni3.Shomari Kapombe4. Aggrey Morris5. Kelvin Yondani6. Frank Domayo7. Mrisho Ngasa8. Sureboy9. Mbwana Samatta10. Amri Kiemba11. Mwinyi Kazimoto

No comments:

Post a Comment