ZANZIBAR MIDIA CORPORATION LTD YAANDA TAMASHA LA WASANII WA ZANZIBAR
Mwenyekiti
 wa Tamasha la tunzo za wasanii bora Zanzibar mwaka 2014/15 Seif Mohd 
Seif akizungumza na waandishi wa habari juu ya maandalizi ya tamasha 
hilo Ofisini kwake mtaa wa Mombasa nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.Picha 
Na Makame Mshenga –Maelezo Zanzibar.
Mratibu 
wa Tamasha hilo Ramadhani Senga akijibu masuala ya waandishi wa habari 
kuhusu tunzo za mwaka huu katika mkutano uliofanyika Jengo la Zanzibar 
Media Corporation Limited mtaa wa Mombasa nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Baadhi ya
 waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo katika jengo la Zanzibar 
Media Corporation Limited wakifuatilia mazungumzo hayo.
Meneja 
Masoko wa Zanzibar Media Corporation Limited Said Khamis akitoa 
ufafanuzi kwa waandishi wa habari katika Mkutano wa maandalizi ya 
Tamasha la tunzo za wasanii bora Zanzibar mwaka huu uliofanyika jengo la
 Zanzibar Media Cortporation Limited mtaa wa Mombasa. Picha Na Makame 
Mshenga –Maelezo Zanzibar.
Taratibu 
za Tamasha la kuwatafuta wasanii bora wa Zanzibar (Zanzibar Music 
Awards) zinazosimamiwa na Kampuni ya Zanzibar Media Corporation 
inayomiliki kituo cha Zenj Fm radio na kitengo cha Zenj Entertainment 
kwa mwaka 2014/2015 zimeanza rasmi leo.
Akizungumza
 na waandishi wa habari katika jengo la Zanzibar Media Corporation, mtaa
 wa Mombasa nje kidogo ya Mji wa Zanzibar, Mwenyekiti wa Tamasha hilo 
Seif Mohd Seif amesema maandali yamekamilika. Amesema tunzo hizo ambazo 
zinalengo la kuwanyanyua wasanii wa Zanzibar kibiashara zitafikia kilele
 chake siku ya Ijumaa tarehe 27.2.2015 katika ukumbi wa Salama Hoteli ya
 Bwawani.
"Lengo la
 tunzo hizi ni kuweza kuwatangaza wasanii wetu wa hapa Zanzibar 
kibiashara, kuona thamani ya kazi zao na mchango wa sanaa zao 
unavosaidia jamii kuipa taaluma kupitia sanaa hizi," alisisitiza Seif 
Mohd Seif.
Ameongeza
 kuwa tamasha la mwaka huu ambalo ni la nane, kama yalivyo matamasha 
yaliyopita yanasaidia kuinua sekta ya utalii kutokana na wageni mbali 
mbali kuhudhuria. Ametoa shukrani kwa wasanii wote wa Zanzibar kwa 
kuonyesha moyo wa kuziimarisha kazi zao ambazo zinakuwa na mvuto kwa 
jamii kwa kuendeleza sanaa nchini.
Pia 
ameipongeza Kamati ya majaji kwa kazi kubwa waliyofanya ya kupitia kazi 
za wasanii, na wadau mbali mbali kutoka vyombo vya habari vya Zanzibar 
ikiwemo Baraza la sanaa kwa michango mikubwa waliyotoa kufanikisha 
maandalizi ya Tamasha hilo.
Mwenyekiti
 wa Zanzibar Music Award amesema katika Tamasha hilo jumla ya makundi 18
 yatawania tunzo hizo kwa wasanii wa Zanzibar pekee.
Ameyataja
 makundi hayo kukwa ni Video bora ya mwaka muziki wa kizazi kipya, video
 bora ya mwaka taarab ya kisasa, Mwanamuziki bora wa mwaka wa hip hop, 
Mwanamuziki wa mwaka wa R&B, Mwanamuziki bora wa Afro pop na 
Mtaarishaji bora wa mwaka.
Wengine 
ni Mwanamuziki bora wa kiume na wa kike taarab ya kisasa, Wimbo bora wa 
taarab ya kisasa ya mwaka, Mwanamuziki bora wa kiume na wa kike taarab 
asilia, Mwanamuziki bora wa kike na kiume muziki wa kizazi kipya na 
wimbo bora wa mwaka wa kizazi kipya.
Katika 
makundi hayo pia kutakuwa na tunzo ya Mwanamuziki bora chipukizi wa 
mwaka, Mwanamuziki bora wa mwaka na Mshairi bora wa mwaka. Seif Mohd 
Seif amewataka watu wote wanaopenda kushiriki tunzo za mwaka huu kuwa 
upigaji wa kura umeanza rasmi leo Jumapili na utamalizika siku ya 
Jumatano tarehe 25.2.2015 na matangazo ya kupiga kura yatarushwa na 
vyombo mbali mbali na katika Gazeti la Nipe Habari na kupitia website 
yaowww.zenjifmradio.com
IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO ZANZIBAR
No comments:
Post a Comment