TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Thursday, February 5, 2015

Burundi: mahakama yaamua Bob Rugurika kusalia jela

Makao makuu ya radio RPA inayoongozwa na mwandishi wa habari, Bob Rugurika, anayezuiliwa katika jela la mkoa wa Muramvya, Burundi.
Mahakama ya jiji la Bujumbura imechukua uamzi wa kumbakiza jela mwanahabari Bob Rugurika, akiwa pia mkurugenzi wa redio RPA, inayosikilizwa na watu wengi nchini Burundi na baadhi ya maeneo ya nchi jirani.
Uamzi huo wa mahakama umekua unasubiriwa ndani ya masaa 48 tangu Jumatatu wiki hii, baada ya mkurugenzi wa redio RPA, kufikishwa mbele ya majaji, katika jela la mkoa wa Muramvya anakozuiliwa. Wanasheria wake wamebaini kwamba watakata rufaa dhidi ya uamzi huo wa Mahakama. Umoja wa Ulaya, Marekani, mashirika ya kimataifa ya haki za binadamu wameitaka serikali kumuachilia huru mwanahabari huyo, kwani hana hatia, huku wakiomba uchunguzi uanzishwe kuhusu watawa 3 kutoka Italia waliouawa mwanzoni mwa mwezi Septemba.
Bob Rugurika alikamatwa na kupelekwa katika jela kuu la Mpimba Jumanne Januari 20 jioni, baada ya kuitika hati iliyotolewa na afisa katika ofisi ya mwendesha mashitaka katika manispaa ya jiji la Bujumbura, Emmanuel Nkurikiye, ambaye alimtaka amfikishe mikononi mwa vyombo vya sheria, mtu mmoja aliyekiri kuhusika na mauaji ya watawa watatu kutoka Italia waliouwawa tarehe 7 na 8 Septemba mwaka 2014, katika wilaya ya Kamenge, kaskazini mashariki mwa mji wa Bujumbura.
Redio RPA iliendesha uchunguzi kuhusu mauaji hayo, na kwa muda wawiki kadhaa redio hio ilikua ikiweka wazi matokeo ya uchunguzi wake, ambapo mtu huyo aliyekiri kuhusika katika mauaji hayo, aliwanyooshea kidole baadhi ya maafisa wakuu katika Idara ya Ujasusi ya Burundi pamoja na polisi, akibaini kwamba wao ndio waliomuagiza akishirikiana na watu wengine (ambao aliwataja majina) kutekeleza mauaji ya watawa hao.
Mtu huyo aliyehojiwa na redio RPA, alimtaja mkurugenzi wa zamani wa Idara ya Ujasusi ya Burundi, jenerali Adolphe Nshimirimana, akibaini kwamba ni mmoja kati ya maafisa wa Idara ya Ujasusi na polisi walioandaa mpango huo wa kuwamalizia maisha watawa hao kutoka Italia.
Hata hivyo katika uchunguzi wake, RPA ilibaini kwamba ilijaribu kuwatafuta watu wote waliotajwa katika kesi hiyo, baadhi walikanausha tuhuma dhidi yao, na wengine walisema kwamba wanasubiri uchunguzi wa vyombo vya sheria vya Burundi.
Akihojiwa na afisa wa Ofisi ya mashitaka, Bob Rugurika alisema, kama chombo cha habari, na kulingana na sheria za uandishi wa habari, RPA iliendesha uchunguzi wake bila hata hivyo kuingilia vyombo vya sheria katika uchunguzi wake, ili kujaribu kutoa mwanga kuhusu mauaji hayo.
Afisa wa Ofisi ya mashitaka anamtuhumu Bob Rugurika kwamba hakutoa ushiriki wake kwa vyombo vya sheria, kuingilia kazi za vyombo vya sheria wakati kesi ikiwa katika hatua ya uchunguzi, na kushiriki katika mauaji ya watawa hao watatu kutoka Italia.
Mkurugenzi wa redio RPA anakabiliwa na kifungo cha miaka 20 jela, iwapo atapatikana na hatia. Baada ya mauaji ya watawa hao, polisi ya Burundi ilimkamata mtu mwenye ugonjwa wa akili, ikimtuhumu kuhusika katika mauaji ya watawa watatu waliouawa tarehe 7 na 8 septemba mwaka 2014 wilayani Kamenge mjini Bujumbura.
Redio RPA imekua ikiendelea kurusha matokeo ya uchunguzi wake, licha ya kuwa mkurugenzi wake anazuiliwa jela.
Kanisa kuu la mjini Bujumbura, Burundi.
flickr
Kanisa Katoliki nchini Burundi inaendela kuomba mkurugenzi huyo wa redio RPA aachiliwe huru, huku ikiomba vyombo vya sheria vya Burundi kuanzisha uchunguzi wa kina ili waliohusika katika mauaji hayo wajulikane, na waadhibiwe kwa mujinu wa sheria.CHANZO:R.F.I

No comments:

Post a Comment