Sheria mpya ya vibali vya ajira yaja

WIZARA ya
 Kazi na Ajira iko katika mchakato wa kuandaa Sheria mpya ya utoaji wa 
vibali vya ajira kwa wageni ili kudhibiti kuajiriwa kwa wageni ili 
kufanya kazi ambazo Watanzania wenyewe wanaweza kuzifanya.
Waziri 
katika wizara hiyo, Gaudentia Kabaka aliliambia Bunge kuwa sheria hiyo 
itatoa mwongozo juu ya utoaji vibali, kwani sasa kumekuwa na sehemu 
nyingi hivyo kuwa na sehemu moja pamoja na adhabu kwa wageni wanaofanya 
kazi zinazoweza kufanywa na Watanzania.
Alisema 
mchakato huo uko karibu kukamilika na utapelekwa bungeni kutokana na 
ratiba na kueleza kuwa itasaidia kudhibiti wafanyakazi wageni wanaoingia
 nchini bila utaratibu maalum na kusababisha kuajiliwa kwenye kazi 
ambazo wenyeji wanaweza kufanya.
Waziri 
alisema hivi karibuni walibaini wageni 300 walioingia nchini kufanya 
kazi katika kiwanda cha saruji cha Dangote, Mtwara kwa kazi zinazoweza 
kufanywa na watanzania.
Wakati 
huo huo, wafanyakazi zaidi ya 350 wa Kampuni ya mgodi wa Bulyanhulu 
waliodai kuachishwa kazi baada ya kupata madhara wakiwa kazini 
wametakiwa kwenda kwenye Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA)
 kupimwa ili kuthibitisha iwapo walipata madhara hayo kutokana na kazi 
walizokuwa wakifanya ili kuweza kutibiwa.
Alisema 
kuwa OSHA ndiyo wenye mamlaka ya kuthibitisha kuwa wafanyakazi hao 
wameathirika na kwa utaratibu walitakiwa kupeleka OSHA barua kutoka kwa 
mwajiri ili kuweza kupimwa na kujua athari walizopata wakiwa kazini 
lakini tangu wafukuzwe kazi mwaka 2007 hawakupeleka barua hiyo.
“Tumegundua
 kuwa wafanyakazi hao hawakuwa na uhusiano mzuri na chama cha 
wafanyakazi hivyo kusababisha ufuatiliaji wa suala hilo kuwa mgumu hivyo
 ninawaagiza kwenda OSHA Dar es Salaam wakapime kwani wako tayari wao 
pamoja na wengine 50 waliofukuzwa “alisema Kabaka.
Pia 
alitaka chama cha wafanyakazi migodini (TAMICO) kuwaunganisha 
wafanyakazi hao ili kufuatilia kwa pamoja na kuepusha kuwa mmoja mmoja.
Mbunge wa
 Kisarawe, Suleiman Jafo (CCM) alisema wafanyakazi hao wamekuwa 
wakihangaika katika ofisi mbalimbali ikiwemo kwenye Wizara ya Kazi na 
Ajira kufuatilia suala hilo.
No comments:
Post a Comment