TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, February 24, 2015

Taarifa kuhusiana na watoto zaidi ya 10 kufariki hospitali ya Amana

icu
Watoto zaidi ya 10 wamefariki dunia baada ya kukosa huduma ya joto katika hospitali ya Amana Jiji Dar es salaam.
Taarifa kutoka hospitalini hapo zinadai waliozaliwa kabla ya wakati  maarufu njiti walifariki dunia February 16 mwaka huu.
Chanzo cha vifo hicyo imetajwa kuwa ni uzembe wa wauguzi baada ya kukatika kwa umeme kwenye chumba walimohifadhiwa.
“Umeme ulikatika muda wa saa 5 asubuhi hadi saa 10 jioni ,wauguzi hawakutekeleza wajibu wao wa kuwaita wazazi wa watoto hao ili wawachukue kwa ajiliya kuwasaidia kupata joto, matokeo yake watoto walifariki dunia” anasema mmoja wa wazazi waliofiwa.
Hata hivyo baadhi ya madaktari wa hospitali hiyo waligoma kuzungumzia na Gazeti la JAMHURI kuhusu suala hilo huku mganga mkuu wa Hospitali hiyo  Dk. Meshack Shimwela akisema taarifa hizo si za kweli na huenda watoto hao walikufa kutokana na matizo menfine kwani wana jenereta za dharura

No comments:

Post a Comment