WAZIRI MEMBE ALIPONGEZA KANISA LA SDA
Waziri wa
 Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Benard Membe akifanya 
mazungumzo na Rais wa Baraza Kuu la Makanisa ya Sabato Duniani Askofu 
Ted Wilson wakati wa siku ya ufungaji wa Kongamano hilo lililofanyika 
Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Waziri wa
 Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Benard Membe ambaye 
alikuwa mgeni rasmi akiwahutubia wananchi pamoja na wageni wengine 
waalikwa (hawapo pichani) wakati wa siku ya ufungaji wa Kongamano hilo 
lililofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Watoto 
wakitoa burudani mbele ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakati wa siku ya
 ufungaji wa Kongamano hilo lililofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es 
Salaam.
Waziri wa
 Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Benard Membe 
(aliyesimama katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya 
viongozi wa Makanisa ya Wasabato (SDA) wakati wa siku ya ufungaji wa 
Kongamano hilo lililofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam siku 
ya tarehe 7 Februari, 2015.
(PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-MAELEZO-DSM)
Na Benedict Liwenga, Maelezo-Dar es Salaam.
WAZIRI wa
 Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe 
amelipongeza Kanisa la Wasabato (SDA) kwa kuwa mfano mzuri wa 
ustahimilivu, uvumilivu wa kidini na imani katika Jamhuri ya Muungano wa
 Tanzania.
Mhe. 
Membe ameyasema hayo leo wakati alipokuwa akifunga rasmi Kongamano la 
siku 4 (4-7 Februari, 2015) Kimataifa la Utume kwa Kanisa la Sabato 
lililofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ambalo lilishirikisha
 Mataifa zaidi ya 20 Duniani.
Alisema 
kuwa, katika kipindi chote cha uongozi wake kama Waziri hajawahi kusikia
 mgogoro wala matatizo yakioongozwa na SDA dhidi ya madhehebu mengine ya
 dini hapa nchini na hata dhidi ya wananchi.
"Mpo 
mnafanya kazi zenu, mnachapa shughuli zenu kwa amani na utulivu, 
hamjachokoza mtu na hiyo ni sifa ya dini mojawapo yenye amani duniani", 
alisema Mhe. Membe.
Alisisitiza
 kwa kuwataka wananchi wa dini zote nchini kuiga mfano wa wana SDA ili 
Tanzania iendelee kuwa nchi yenye amani na utulivu.
Aidha, 
alieleza kuwa, Dini na Diplomasia vina husiana pale masuala ya amani, 
ulinzi na usalama yanapoguswa huku akiwataka wananchi wa dini zote 
nchini kushiriki katika kutengeneza viongozi bora katika jamii kwa 
misingi ya uadilifu ambao watasimamia amani na kujiepusha na vitendo 
viovu ikiwemo rushwa.
Aliongeza
 kuwa dhamira ya Serikali ya kuendelea kushirikiana nalo kwa ajili ya 
ustawi wa nchi huku akieleza kuwa, Serikali itaendelea kulinda uhuru wa 
kuabudu kwa dini zote kama inavyoelezwa kwenye Katiba ya Jamhuriu ya 
Muungano wa Tanzania.
Naye Rais
 wa Baraza Kuu la Makanisa ya Sabato Duniani, Askofu Ted Wilson alisema 
kuwa anawaombea Viongozi wa Tanzania waendelee na maono kwa lengo la 
kuwatumikia wananchi na kwamba wakimtumaini Mungu atawawezesha kupata 
maono mapya kwa ajili ya kulitumikia Taifa zima.
Kongamano
 hilo lilishirikisha Mataifa zaidi ya 20 ambapo Kanisa hilo la Wasabato 
ni Kanisa linalokua duniani likiwa na Waumini milioni 307 huku Waumini 
milioni 30 wakiwa Afrika na takriban milioni 5 wakiwa Tanzania.
No comments:
Post a Comment