TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, February 24, 2015

Watanzania sasa Kupatiwa Viza Huko Huko India 


Wasafiri kutoka Tanzania kwenda India kwa  shughuli za matibabu na biashara wataruhusiwa  kupata visa wafikapo nchini humo.

Hayo yalisemwa na Balozi wa India nchini, Debnath Shaw wakati akijibu maswali ya wafanyabiashara wa kitanzania wakati wa mkutano baina ya wafanyabiashara wa ndani na wenzao kutoka jimbo la Gujarat India.
 
Alisema: “Tutahakikisha tunafanya utaratibu huo na utaanza siku za usoni ili kupunguza usumbufu wanaoupata Watanzania waendao India”.
 
Kwa upande wake, Ofisa Mkuu Mtendaji wa Global  Investors Consultstion Center (GICC), Shainul Bhanji alisema kutokana na ripoti ya Benki ya Dunia Tanzania imeonekana kuwa ni nchi yenye mazingira mazuri ya biashara kwani ripoti inaonesha Tanzania inaendelea kushika nafasi nzuri ukilinganishwa na nchi jirani za Kenya na Uganda.
 
“Tanzania ilikuwa nafasi  ya 142 kati ya 180 kwa mwaka 2011 lakini sasa imepanda hadi nafasi ya 131  huku Kenya ikiwa katika nafasi ya 136 na Uganda nafasi ya 132,” alisema Bhanji.
 
Naye Rais wa Taasisi ya Wenye Viwanda toka Jimbo la Gujarat India Amit Patel alisema kwa sasa India ni nchi ya nne kwa ukubwa kwa nchi zinazofanyabiashara kwa Afrika na wana uhakika kuwa watafanyabiashara kuzidi China, Marekani na Ulaya.
 
Alisema Serikali ya India imeahidi kutoa mikopo ya masharti nafuu ya bilioni 6 mwaka huu kwa nchi za Afrika ili kuboresha miundombinu na mazingira ya kufanyabiashara.
 
Naye Mwenyekiti wa wafanyabiashara, wakulima na wenye viwanda nchini Francis Lukwaro alisema mkutano utasaidia wafanyabiashara wa Tanzania kujifunza mambo mapya ya kibiashara kutoka India.
 
Alisema kwa upande wa Tanzania kuna mengi ya kujifunza kutoka kwa wafanyabiashara hawa kwani wengi wao ni wafanyabiashara wakubwa na wameendelea.

No comments:

Post a Comment