Fedha Zakwamisha kukamilika Mradi wa DART
Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka Dar es Salaam (DART) unakabiliwa na changamoto ya kifedha katika ujenzi wa miundombinu, kutokana na ongezeko la mahitaji ya fedha za kuukamilisha.
Bunge
 lilielezwa kwamba ongezeko la mahitaji ya fedha za kukamilisha mradi 
huo ni Sh bilioni 64.7, ambazo kati yake Sh bilioni 20.6 ni ongezeko la 
mishahara na Sh bilioni 44.1 ni ongezeko la kazi na madai mengine.
Mjumbe
 wa Kamati ya Bunge ya Tawala za Mikoa  na Serikali za Mitaa, Dk Athuman
 Mfutakamba alisema hayo jana wakati akiwasilisha taarifa ya mwaka ya 
kamati kuanzia Januari 2014 hadi 2015. 
Kamati 
 hiyo imeishauri serikali kufanya jitihada za makusudi, kuhakikisha 
mradi unaendelea kutekelezwa kama ilivyopangwa na fedha yote 
inayohitajika kukamilisha hatua mbalimbali za mradi, zinatengwa na 
kupelekwa hatua zikamilike kwa wakati. 
Kwa
 mujibu wa Mfutakamba, inadaiwa ongezeko hilo limefanya mkandarasi 
kutoonesha utayari wa kuanza kazi katika barabara ya Msimbazi kwa hofu 
ya kutokuwepo kwa fedha za kumlipa. 
Changamoto
 nyingine ambayo wabunge walielezwa kwamba inakabili mradi, ni uharibifu
 wa miundombinu ambao baadhi ya wananchi na wafanyabiashara ndogo 
huvamia maeneo ya ujenzi yanayoendelea.
Vile vile kumekuwapo tabia ya wizi wa samani za barabara, mifuniko ya maji ya mvua, maji taka na huduma nyingine. 

No comments:
Post a Comment