NSSF YAANZA MCHAKATO WA KUWASAKA WENYE VIPAJI VYA MPIRA WA MIGUU

Itakumbukwa
 kuwa mnamo tarehe 26/01/2015 Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii 
(NSSF) lilisaini mkataba maalum na timu ya Real Madrid ya Nchini 
Hispania ya kuanzisha na kuendesha kituo cha michezo (NSSF- REAL MADRID 
Sports Academy) kwa lengo la kuibua, kuendeleza na kukuza vipaji kwa 
mpira wa miguu.
Shirika 
la NSSF litajenga kituo hicho katika eneo la Mwasonga Kigamboni nje 
kidogo ya mji wa Dar es Salaam na wataalamu kutoka timu ya Real Madrid 
watatoa mafunzo kwa vijana wa umri wa miaka13 hadi 19 kwa madhumuni ya 
kukuza mpira wa miguu nchini, kupata wachezaji bora wanaouzika nje na 
ndani ya nchi pamoja na kulipatia mapato shirika na nchi kwa ujumla .
Akizungumza
 na Waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya Habari Nchini, Mkurugenzi 
Mkuu wa Shirika hilo Dr. Ramadhani K. Dau alisema mradi huo ukiwa kama 
sehemu ya uwekezaji wa NSSF ulianza maramoja baada ya kusaini mkataba.
NSSF 
imeanza utaratibu wa kuwabaini vijana walengwa ambapo kwa kuanzia 
utafutaji wa vipaji vya mpira wa miguu utaanzia mkoa wa Dar es Salaam 
kwa vijana wenye umri wa chini ya miaka 14. Utafutaji wa vipaji 
utafanyika kiwilaya kwa Wilaya za mkoa wa dar es salaam na utakuwa 
unafanyika katika viwanja vya Karume. Zoezi hilo litakuwa linafanyika 
kati ya saa 1 asubuhi hadi saa 9 alasiri kwa tarehe zilizoainishwa.
Uandikishaji
 wa washiriki utakuwa unafanyika siku za mwisho wa wiki ili kutoathiri 
wanafunzi watakaopenda kushiriki na utaanza rasmi tarehe 14 na 15,na 
tarehe 22 na 23 Februari 2015, na kufuatiwa na michezo ya majaribio 
tarehe 28 Februari,na Tarehe 1 Machi 2015 kwa wilaya zote za mkoa wa Dar
 es salaam ambapo kituo kitakuwa viwanja vya Karume kuanzia saa moja 
asubuhi hadi saa 9 alasiri.
Zoezi la 
Uandikishaji halitahusisha gharama zozote kwa washiriki, na uandikishaji
 wa washiriki utafanyika kwa kujaza fomu maalum na kupewa namba ya 
ushiriki na kila mshiriki atapata fursa ya kucheza katika awamu mbili za
 dakika 30. Kwa kuanzia washiriki watatakiwa kuja na vifaa vyao vya 
michezo.
Zoezi la 
awali litafanywa na wataalam wa ndani ya nchi ambapo Vijana 500 kati ya 
wote watakaofanyiwa majaribio wataingia katika awamu ya pili ya 
majaribio na watadahiliwa na wataalamu kutoka Klabu ya Real Madrid na 
hatimaye kupatikana vijana 30 amabo ndio wataingia katika shule maalum 
ya mafunzo kwa awamu ya kwanza.
Wakati wa
 uandikishwaji washiriki watatakiwa kuja na wazazi/walezi wao wakiwa na 
vitambulisho vyao,na kijana husika awe na Cheti halisi cha kuzaliwa na 
kopi yake pamoja na picha mbili za pasport rangi ya blue.Muda wa 
uandikishaji na majaribio unaweza kuongezwa kulinagana na mahitaji.
Shirika 
la NSSF linatoa wito kwa vijana kujitokeza kwani ni fursa kwao ya kuweza
 kujiendeleza kimichezo na kujiajiri katika tasnia hiyo
No comments:
Post a Comment