TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Friday, February 27, 2015

KIKWAZO CHA UKAWA KUSIMAMISHA MGOMBEA MMOJA WA URAIS

Stori: mwandishi wetu
PRESHA inazidi kuongezeka kila kukicha kuelekea kwenye uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba, 2015 ambapo sarakasi mbalimbali za kisiasa zinaendelea kuchezwa na wafuasi wa vyama vyote bila kujali chama tawala au vyama vya upinzani.
Uwazi Mizengwe limebaini kuwa macho na masikio ya wengi, yameelekezwa kwenye muungano wa vyama vinne vya kisiasa vya upinzani, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Chama cha Wananchi (CUF), NCCR Mageuzi na NLD vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
WANANCHI WANASEMAJE?
Uwazi Mizengwe liliingia mitaani kujaribu kutafuta mawazo ya wengi.
"Ni dhahiri kwamba suala la Ukawa kumsimamisha mgombea mmoja haliwezekani, lazima dakika za mwisho Ukawa watavurugana," alisema Saleh Kiwia, mkazi wa Jiji la Dar es Salaam.

Uwazi halikuishia hapo, liliendelea kudodosa huku na kule na kubaini kuwa suala la Ukawa kumsimamisha mgombea mmoja katika nafasi ya urais, ni gumu kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo nguvu iliyonazo chama kimojakimoja, wafuasi na ushawishi kwa wananchi.
"Kwa ushawishi na nguvu ilizonazo Chadema, haitakuwa rais kwa chama kingine kumsimamisha mgombea upande wa Bara wakati tayari wapo Freeman Mbowe na Dokta Wilbroad Slaa ambao wana ushawishi mkubwa miongoni mwa wapiga kura," alisema msomaji mwingine kwa sharti la kutoandikwa jina lake gazetini.
LIPUMBA TAYARI AMESHATANGAZA NIA
Wakati vuguvugu hilo likiendelea, hivi karibuni CUF kiliitisha mkutano na waandishi wa habari ambapo pamoja na mambo mengine, kilimtangaza mwenyekiti wake wa taifa, Ibrahim Lipumba kuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Uchaguzi wa CUF, Shaweji Mketo, alinukuliwa akisema: "Kwa upande wangu mie kama mkurugenzi wa uchaguzi nina imani na Profesa Lipumba, kuwa hatakuwa ndiye mgombea wetu wa urais tu kwa CUF bali hata kwa upande wa Ukawa,"alisema Mketo.
Kauli hiyo ilipokelewa kwa hisia tofauti miongoni mwa wafuasi wa vyama hivyo vya siasa, kila mmoja akizungumza lake."Haiwezekani Lipumba ndiyo awe mgombea wa Ukawa kwa sababu Chadema ndiyo chenye nguvu upande wa Bara," alikaririwa Dickson Mapunda, mfanyabiashara wa Soko la Kariakoo.
MASHARTI YA CHADEMA KWA VYAMA VINGINE
Duru nyingine za kisiasa kutoka ndani ya Chadema, zinaeleza kwamba chama hicho hakiwezi kukubali kuona mgombea kutoka chama kingine anasimama kuwania nafasi ya urais kwa sababu chenyewe ndiyo chenye nguvu, mtandao mpana na wafuasi wengi kwa hiyo ni lazima kitoe mgombea.

"Masharti makubwa ya Chadema kwa vyama vingine ni kwamba lazima vikubaliane kumuunga mkono mgombea atakayetoka kwenye chama hicho, jambo ambalo halitakuwa rahisi kwa sababu tayari CUF wameshaonesha wanataka nani ndiyo awe mgombea, lazima watavurugana tu," alikaririwa Mwanaisha Mataka, mkazi wa Kinondoni.CHANZO:Globalpublishers

No comments:

Post a Comment