HUAWEI NA UMOJA WA AFRIKA ZASAINI MAKUBALIANO

Makamu wa
 Rais wa kampuni ya Huawei katika idara inayohusika na mahusiano ya 
serikali Ulimwenguni, Bw. David Harmon (wapili kushoto) akipeana mkono 
na Makamu Mweyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika Bw. Erastus Mwencha 
(wapili kulia), mara baada ya kusaini makubaliano yatakayosaidia 
kuongeza ushirikiano baina yao katika kuimarisha maendeleo katika 
miundombinu ya teknolojia ya Habari na Mawasiliano (teknohama).
 Hafla ya kusaini makubaliano hayo ilifanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia. Wakishuhudia ni wawakilishi kutoka pande zote mbili.(V.S)
Kampuni 
ya Huawei Technologies inayoongoza katika sekta ya habari na mawasiliano
 duniani, imesaini makubaliano (MoU) na Umoja wa Afrika (AU), 
makubaliano yatakayosaidia kuongeza ushirikiano baina yao katika 
kuimarisha maendeleo katika miundombinu ya teknolojia ya Habari na 
Mawasiliano (teknohama).
Makubaliano
 hayo yalisainiwa hivi karibuni mjini Addis Ababa, Ethiopia kwenye 
Mkutano wa AU wa mwaka 2015 ambao pamoja na mambo mengine ulijadili pia 
namna ya kuimarisha uelewa wa teknolojia ya Habari na Mawasiliano 
(teknohama) kwa nchi wanachama sambamba na kujenga uwezo wa juu katika 
maendeleo ya miundombinu ya teknolijia hiyo.
Akizungumza
 kwenye mkutano huo, Makamu mweyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika 
Bw. Erastus Mwencha alisema maendeleo ya Teknolojia ya Habari na 
Mawasiliano (teknohama) yana msaada mkubwa kwa ukuaji wa uchumi 
ulimwenguni na pia ni nguzo muhimu katika kuleta madadiliko chanya 
kwenye setka mbalimbali.
"Maendeleo
 ya teknolojia hii yataleta mabadiliko makubwa sana katika sekta 
mbalimbali na ndio maana tunatafuta washirika wanaoweza kufanya kazi na 
sisi ili kufanikisha hilo. Huawei kama kampuni imara kwenye teknolojia 
hiyo tunaamini pia itakuwa ni msaada mkubwa itakapo shirikiana na 
sisi...tunafurahi kuwa nao kwenye huu mradi,'' alisema Mwencha.
Kwa 
upande wake, Makamu wa Rais wa kampuni ya Huawei katika idara 
inayohusika na mahusiano ya serikali Ulimwenguni, Bw. David Harmon 
alisema kampuni yake ina nia yakukuza kimataifa maendeleo sekta ya 
teknohama na ndiyo maana kwa muda mrefu imekuwa ikisaidiana na serikali 
mbalimbali katika kuimarisha miundombinu inayohusiana na sekta hiyo.
"Huawei 
ina jukumu la kuhakikisha tunashikirikaina na washirika wetu kwenye 
nyanja zote za teknohama ili kujenga Afrika bora yenye kushikamana, kwa 
sababu tunaamini kwamba teknolojia ICT, hasa mawasiliano ya simu ni 
nguzo muhimu si tu kwa Afrika bali ulimwenguni wote.
"Kwa 
miaka yetu 17 ya uzoefu katika sekta ya teknohama sambamba na mtandao wa
 kimataifa ulimwenguni kote ina maana kwamba Huawei ipo katika nafasi 
nzuri ya kushiriki kwenye namna bora ya kutafuta ufumbuzi kwa masuala ya
 teknohama. Tupo tayari kubadilishana uzoefu wetu na Umoja wa Afrika, " 
Harmon aliongeza.
No comments:
Post a Comment