TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, February 3, 2015

HUAWEI NA UMOJA WA AFRIKA ZASAINI MAKUBALIANO


Makamu wa Rais wa kampuni ya Huawei katika idara inayohusika na mahusiano ya serikali Ulimwenguni, Bw. David Harmon (wapili kushoto) akipeana mkono na Makamu Mweyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika Bw. Erastus Mwencha (wapili kulia), mara baada ya kusaini makubaliano yatakayosaidia kuongeza ushirikiano baina yao katika kuimarisha maendeleo katika miundombinu ya teknolojia ya Habari na Mawasiliano (teknohama).
Hafla ya kusaini makubaliano hayo ilifanyika mjini Addis Ababa, Ethiopia. Wakishuhudia ni wawakilishi kutoka pande zote mbili.(V.S)
Kampuni ya Huawei Technologies inayoongoza katika sekta ya habari na mawasiliano duniani, imesaini makubaliano (MoU) na Umoja wa Afrika (AU), makubaliano yatakayosaidia kuongeza ushirikiano baina yao katika kuimarisha maendeleo katika miundombinu ya teknolojia ya Habari na Mawasiliano (teknohama).
Makubaliano hayo yalisainiwa hivi karibuni mjini Addis Ababa, Ethiopia kwenye Mkutano wa AU wa mwaka 2015 ambao pamoja na mambo mengine ulijadili pia namna ya kuimarisha uelewa wa teknolojia ya Habari na Mawasiliano (teknohama) kwa nchi wanachama sambamba na kujenga uwezo wa juu katika maendeleo ya miundombinu ya teknolijia hiyo.
Akizungumza kwenye mkutano huo, Makamu mweyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Bw. Erastus Mwencha alisema maendeleo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (teknohama) yana msaada mkubwa kwa ukuaji wa uchumi ulimwenguni na pia ni nguzo muhimu katika kuleta madadiliko chanya kwenye setka mbalimbali.
"Maendeleo ya teknolojia hii yataleta mabadiliko makubwa sana katika sekta mbalimbali na ndio maana tunatafuta washirika wanaoweza kufanya kazi na sisi ili kufanikisha hilo. Huawei kama kampuni imara kwenye teknolojia hiyo tunaamini pia itakuwa ni msaada mkubwa itakapo shirikiana na sisi...tunafurahi kuwa nao kwenye huu mradi,'' alisema Mwencha.
Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa kampuni ya Huawei katika idara inayohusika na mahusiano ya serikali Ulimwenguni, Bw. David Harmon alisema kampuni yake ina nia yakukuza kimataifa maendeleo sekta ya teknohama na ndiyo maana kwa muda mrefu imekuwa ikisaidiana na serikali mbalimbali katika kuimarisha miundombinu inayohusiana na sekta hiyo.
"Huawei ina jukumu la kuhakikisha tunashikirikaina na washirika wetu kwenye nyanja zote za teknohama ili kujenga Afrika bora yenye kushikamana, kwa sababu tunaamini kwamba teknolojia ICT, hasa mawasiliano ya simu ni nguzo muhimu si tu kwa Afrika bali ulimwenguni wote.
"Kwa miaka yetu 17 ya uzoefu katika sekta ya teknohama sambamba na mtandao wa kimataifa ulimwenguni kote ina maana kwamba Huawei ipo katika nafasi nzuri ya kushiriki kwenye namna bora ya kutafuta ufumbuzi kwa masuala ya teknohama. Tupo tayari kubadilishana uzoefu wetu na Umoja wa Afrika, " Harmon aliongeza.

No comments:

Post a Comment