TIC YAKUTANA NA UJUMBE WA WAFANYABIASHARA KUTOKA NCHINI UJERUMANI

Mkurugenzi
 Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC),Juliet Kairuki (wa pili 
kushoto) akizungumza katika mkutano maalum kati ya Uongozi wa TIC na 
ujumbe wa wafanyabiashara kutoka nchini Ujerumani,wenye lengo la 
kuhamasisha na kukuza Uwekezaji na biashara kati ya Tanzania na 
Ujerumani,uliofanyika jana jioni kwenye ukumbi wa Mikutano ya kituo 
hicho,jijini Dar es salaam.Ujumbe huo unaongozwa na Waziri wa Masuala ya
 Kiuchumi na Nishati wa nchini Ujerumani,Mh. Matthias Machnig (wa pili 
kulia)

Mratibu 
wa Uwekezaji wa Kimataifa wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC),Zacharia
 Kingu akifafanua jambo wakati akiwasilisha taarifa ya uwekezaji katika 
maeneo mbali mbali nchini wakati wa mkutano maalum kati ya Uongozi wa 
TIC na ujumbe wa wafanyabiashara kutoka nchini Ujerumani,wenye lengo la 
kuhamasisha na kukuza Uwekezaji na biashara kati ya Tanzania na 
Ujerumani,uliofanyika jana jioni kwenye ukumbi wa Mikutano ya kituo 
hicho,jijini Dar es salaam.

Ujumbe wa
 wafanyabiashara kutoka nchini Ujerumani pamoja uongozi wa TIC 
ukifatikia kwa makini taarifa ya uwekezaji iliyokuwa ikitolewa na 
Mratibu wa Uwekezaji wa Kimataifa wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania 
(TIC),Zacharia Kingu (kushoto).

Mkurugenzi
 Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC),Juliet Kairuki 
(katikati) akitoa ufafanuzi wa maswala mbali mbali ya uwekezaji kwa 
ujumbe wa wafanyabiashara kutoka nchini Ujerumani waliotembelea kituo 
hicho jana jioni,jijini Dar es salaam.

Kiongozi 
wa Msafara wa Wafanyabiara hao ambaye ni Waziri wa Masuala ya Kiuchumi 
na Nishati wa nchini Ujerumani,Mh. Matthias Machnig akizungumza na 
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC),Juliet 
Kairuki.

Meneja wa
 Kitengo cha Uratibu Miradi ya Ubia (Sekta ya Umma na Binafsi) wa 
TIC,Said Amir akitoa ufafanuzi juu ya maswala ya ubia katika 
miradi,wakati wa mkutano maalum kati ya Uongozi wa TIC na ujumbe wa 
wafanyabiashara kutoka nchini Ujerumani,wenye lengo la kuhamasisha na 
kukuza Uwekezaji na biashara kati ya Tanzania na Ujerumani,uliofanyika 
jana jioni kwenye ukumbi wa Mikutano ya kituo hicho,jijini Dar es 
salaam.

Kaimu 
Mkurugenzi wa Masuala ya Ushirika wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania 
(TIC),Revocatus Arbogust akichangia jambo katika mkutano huo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha 
Uwekezaji Tanzania (TIC),Juliet Kairuki (wa pili kushoto) akiongea na 
ujumbe huo wakati akiwaonyesha moja ya Jengo lilalotumiwa Kituo hicho lililojengwa na Wajerumani.
No comments:
Post a Comment