Wasichana London wajiunga na IS Syria

Uturuki 
imeshutumu Uingereza kwamba imechukua muda mrefu kuijulisha nchi hiyo 
kuhusu wanafunzi wa kike watatu waliokuwa wakisoma London Uinger kwamba 
walisafiri kwenda nchini Syria kwa lengo la kujiunga na Islamic State.
Inaelezwa
 kuwa wanafunzi hao walipanda ndege ya shirika la ndege la Uturuki 
kutoka Uingereza na walihitaji hati ya kusafiri na visa kuingia Uturuki.
 Sakata la wanafunzi hao wa kike kutoka London kwenda kujiunga na 
wapiganaji wa Islamic State limekuwa limeshtua wengi.
Huku 
serikali ya Uturuki inasema ingechukua hatua kama ingepewa taarifa 
mapema Naibu Waziri Mkuu wa Bulent Arinc anatupa lawama moja kwa moja 
kwa Uingereza kwamba iliichelewa kuijulisha nchi hiyo kabla ya wanafunzi
 hao hawajaingia katika mji mkuu wa Instanbul.
"Tumefuatilia
 na tumezuia watu wapatao elfu kumi ambao hapo awali waliripotiwa kwetu 
kutaka kuingia Uturuki kwa tuhuma za kutaka kuendesha shughuli za 
kigaidi. Tumetimiza wajibu wetu. Kama Serikali ya Uingiereza 
ingetujulisha mapema maafisa wetu wa usalama wangechukua hatua 
madhubuti. Tunaamini kuna haja ya kuanganisha nguvu kwa pamoja ili 
kuratibu na kupambana na ugaidi." Alisema.
Wakati 
kukiwa na taarifa hizo za wanafunzi wa kike waliokuwa wakisoma London 
Uingereza kuingia nchini Syria kujiunga na Islamic State
Nayo 
serikali ya Ufaransa kwa mara ya kwanza imezikamata hati za kusafiria za
 raia wapatao sita ambao wanatuhumiwa kwenda nchini Syria kujiunga na 
wapiganaji hao wa Islamic State.
Waziri wa
 Mambo ya ndani wa ufaransa Benard Cazeneuve amesema kitengo cha ujasusi
 kinaamini kwamba watu hao walikuwa na mpango wa kusafiri na kwamba 
swala hilo linahusiana na mambo ya usalama.
"Tunaamini
 hatua hizi zilizochukuliwa zimefanikiwa kwa sababu kama raia wa 
Ufaransa watakwenda kupigana Iraq na Syria watasababisha hatari kubwa 
kwa usalama wa taifa wakati watakaporudi. Wanaweza kuendesha vitendo vya
 kigaidi kwa kiwango kikubwa." Alisema.CHANZO:BBC
No comments:
Post a Comment