TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, February 24, 2015

Kilichowapata wanafunzi hawa baada ya kuudhihaki utawala wa mfalme wao

thai 
Wanafunzi wawili nchini Thailand wamehukumiwa kukaa gerezani kwa muda wa miaka miwili na nusu kwa kosa la kuudhihaki utawala wa kifalme wa nchi hiyo kupitia mchezo wa jukwaani katika chuo kikuu cha Thammasat jijini Bankok.
Wanafunzi hao Patiwat Saraiyaem (23) na Porntip Mankong (26) walihukumiwa jana walipokutwa na hatia ya kutunha igizo walilolipa jina la ‘The Wolf Bridge‘ mwaka jana ambapo wasaidizi wa mfalme walisema imeudhihaki utawala wake.
Awali wanafunzi hao walihukumiwa kifungo cha miaka mitano kila mmoja lakini walipunguziwa hadi miaka miwili na nusu baada ya kukiri kosa.
Thai King Bhumibol Adulyadej of Thailand surrounded by his family members
“Mahakama ijejiridhisha kuwa ushiriki wao katika mchezo wa jukwaani umeudhalilisha utawala wa kifalme, lakini baada ya kuirahisishia mahakama kwa kukiri kosa tuliamua kuwaounguzia kifungo“alisema Jaji wa Mahakama.
Inasemekana sababuza kutunga igizo hilo ni kusherehekea miaka 40 ya wanafunzi wachuo hicho kupigwa na wanajeshi wa Taifa hilo mwaka 1973 walipoandamana kudai demokrasia.

No comments:

Post a Comment