TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Tuesday, February 24, 2015

Raia sita wa Ufaransa wanyang'anywa pasipoti 

Mpiganaji wa Dola la Kiislam akishikilia bendera nyeusi ya Dola la Kiislam katika mji wa Racca (Syria) Juni 29 mwaka 2014.
Uamzi huo umechukuliwa na kutangazwa na wizara ya ya mambo ya ndani, ambayo imethibitisha kwamba watu hao sita wamekua wakijiandaa kusafiri kutoka Ufaransa kuelekea Syria.
Uamzi huo unaendana sambamba na sheria dhidi ya ugaidi iliyopitishwa mwaka 2014.
Uamzi uliyochukuliwa na wizara ya mambo ya ndani dhidi ya watu hao sita inapiga marufuku watu hao kusafiri nje ya Ufaransa. Utaratibu huu unaendana na sheria iliyopitishwa Novemba mwaka 2014, ambayo inapiga marufuku raia wa Ufaransa kusafiri kwenda Syria.
Ni wiki moja sasa, Waziri mkuu wa Ufaransa, Manuel Valls, alitoa takwimu ya kuvutia, ambayo inaeleza kuwa idadi kubwa ya raia wa Ufaransa wamejiunga na makundi ya kijihadi. kwa mujibu wa Waziri mkuu, karibu raia 1400 wa Ufaransa wamekua na mawasiliano na makundi ya wanajihadi ambayo yanahusika na kuwaajiri na kuwapeleka watu katika makundi hayo kijihadi hususan kundi la Dola la Kiislamu linaolodhibiti baadhi ya maeneo ya Syria na Iraq.
Watu hao sita wana umri uliyo kati ya 23 na 28, na ni wakazi wa eneo la kusini mashariki mwa Ufaransa. Baadhi yao walishajielekeza nchini Syria katika miaka iliyopita.
Kwa mujibu wa wizara ya mambo ya ndani, watu hao sita, ikiwa ni pamoja na wanaume na wanawake wamekua wakijiandaa kusafiri ili kujiunga na kundi la wanamgambo wa Dola la Kiislamu.CHANZO:R.F.I

No comments:

Post a Comment