TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, November 17, 2014

Unajua sala aliyoifanya Mike Sonko pamoja na ujumbe alioutoa kwa wanaowachania nguo wasichana?

Sonko 
Jina la Mbunge wa Jimbo la Makadara Kenya, Mike Sonko sio jina geni, wengi tunamfahamu kutokana na vitu vingi ambavyo amekuwa akifanya ikiwa ni pamoja na aina ya maisha anayoishi na amekuwa akisifiwa kutokana na namna ambavyo amekuwa akiwajibika kwa wananchi wake anaowaongoza.
Stori kutoka Kenya ambayo imetawala vyombo vingi vya habari ni kuhusiana tukio la msichana kuchaniwa nguo na wanaume hadharani kutokana na kuvaa vibaya.
Ujumbe aliouandika Sonko kutokana na tukio ulianza na sala hii; “…. Namuomba Mungu awasamehe wanaume wanaowachania nguo wasichana.. Namuomba awaeleweshe wote kwamba wasichana wa karne ya 21 wako kidijitali sana na tofauti…
…. Namuomba atutawale sote na kuirejesha amani kati ya wanaume hao na wanawake waliochaniwa nguo.. Leta amani kwa wasichana waliochaniwa nguo wakidhania mavazi hayo yanasababisha waaibishwe kwa kujua ama kutokujua…”– Sonko
Sonko II
Baada ya sala hiyo, Sonko alitangaza kutoa zawadi ya fedha kiasi cha shilingi 100,000/= za Kenya kwa mtu atakayetoa taarifa zitakazopelekea kukamatwa wale wote waliohusika kufanya kitendo hicho cha kikatili katika mitaa ya Nairobi.

No comments:

Post a Comment