TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Wednesday, November 12, 2014

Soma kuhusu binti aliyeamua kuongeza titi la tatu katika mwili wake

tt
Kweli duniani kuna vituko na ndivyo ilivyotokea kwa binti mmoja mwenye umri wa miaka21 baada yakufanyiwa upasuaji wa kuongeza titi la tatu katika mwili wake.
Binti huyo aliyejulikana kama Jasmine Tridevil alitumia pauni 12,000 za kimarekani sawa na zaidi ya milioni20 za kitanzania kwa ajili ya kufanya upasuaji ili  mradi aongeze kiungo hicho.
Katika makala iliyoandikwa na Gazeti la JAMBOLEO msichana huyo kutoka Marekani alisema kuwa alianza kuhifadhi fedha kwa ajili ya upasuaji huo kwa miaka miwili iliyopita ilimradi atimize azma yake.
Madaktari waliomfanyia upasuaji huo walikata sehemu ya nyama ya tumbo lake kwa ajili ya kupachika kiungo alichokua akikitaka katika sehemu ya kifua chake.
Awali aliita zaidi ya madaktari 50 ili kufanya zoezi hilo lakini walikataa kumfanyia upasuaji huo na ndipo baadhi ya madaktari wakajitokeza na kukubali.
Hata hivyo kwa mujibu wa mmoja wa madaktari hao alisema titi la tatu halitakua na uwezo wa kufanya kazi kama yalivyo mengine mawili ila kikubwa anapenda kuwa katika hali hiyo.
Akizungumzia hatua ya wazazi wake baada ya kitendo chake alisema kuwa hawakupendezwa nacho hadi kufikia hatua ya kukataa kuongea naye kabisa

No comments:

Post a Comment