TIFFAN ENT

TIFFAN ENT

TUKO WANGAPI

TUKO WANGAPI

GLORY FREIGHT

GLORY FREIGHT

Monday, November 3, 2014

Hivi ndivyo alivyouawa nahodha wa timu ya taifa ya Afrika Kusini, azikwa kishujaa

senzo 8 
Mazishi ya aliyekuwa nahodha wa Afrika Kusini Senzo Robert Meyiwa yamefanyika Jumamosi Novemba 1 baada ya kuuawa na majambazi waliovamia nyumbani kwa mchumba wake, Kelly Khumalo .
Orlando Pirates
Mwenyekiti wa klabu Ya Orlando Pirates, Irvin Khoza akitoa heshima za mwisho kwenye mazishi ya Senzo.
Eneo la makaburini alikozikwa Senzo Meyiwa huko Kwazulu Natal , Afrika Kusini.
Eneo la makaburi ya mashujaa alikozikwa Senzo Meyiwa, Kwazulu Natal , Afrika Kusini.
Taarifa ya namna mauaji hayo yalivyotokea imetolewa, ambapo imesemekana Senzo alikuwa akijiandaa kutoka kwenye nyumba ya mama mzazi wa Kelly Khumalo wakati majambazi watatu walipovamia nyumba hiyo wakiwa na bastola, wakiwaamuru waliomo ndani ya nyumba hiyo kutoa vitu vya thamani walivyonavyo ikiwemo simu za mkononi na fedha.
Senzo alikuwa akicheza na mtoto wake ndani ya chumba, alitoka kuja sebuleni baada ya kusikia kelele za majambazi hao wakati mpenzi wa Senzo alikimbilia chumbani nakujifungia.
Jambazi mmoja alifyatua risasi chini baada ya kushindwa kuufungua mlango alimojifungia Kelly.
Senzo akiwa kwenye harakati za kutoka nje ya mlango kufukuzana na jambazi mwingine alipigwa risasi mgongoni iliyopelekea mauti yake.
Umati wa watu waliojitokeza kushuhudia mazishi ya Senzo Meyiwa .
Umati wa watu waliojitokeza kushuhudia mazishi ya Senzo Meyiwa, Kwa Zulu Natal.

No comments:

Post a Comment